Scripture Stories
Sura ya 14: Nabii na Ufunuo kwa ajili ya Kanisa: Septemba 1830


Sura ya 14

Nabii na Ufunuo kwa ajili ya Kanisa

Septemba 1830

Picha
ubatizo
Picha
Hiram Page akiwa ameshikilia jiwe

Joseph na Emma Smith walihamia tena New York. Mtu mmoja aliyeitwa Hiram Page aliishi huko. Alikuwa muumini wa Kanisa. Alikuwa na jiwe ambalo alisema lilimsaidia kupokea ufunuo kwa ajili ya Kanisa.

Mafundisho na Maagano 28, kichwa cha habari cha sehemu

Picha
Joseph akizungumza na Hiram Page

Waumini wengi wa Kanisa walimwamini Hiram Page, akiwemo Oliver Cowdery. Baadhi ya watu walidhani Hiram Page alikuwa nabii.

Mafundisho na Maagano 28, kichwa cha habari cha sehemu

Picha
Joseph anapokea ufunuo

Oliver alimwuliza Joseph kuhusu Hiram Page. Joseph aliomba, na Yesu alimpa ufunuo. Yesu alisema kwamba mtu mmoja tu ndiye angeweza kupokea ufunuo kwa ajili ya Kanisa lote. Mtu huyo alikuwa Nabii Joseph Smith.

Picha
Joseph akimfariji Oliver

Yesu alisema kwamba Oliver na wengine wangeweza kupokea ufunuo kwa ajili yao wenyewe, lakini si kwa ajili ya Kanisa lote. Oliver alimwamini Joseph. Alijua kwamba ufunuo wa Hiram Page haukuwa sahihi.

Picha
Oliver akizungumza na Hiram Page

Yesu alimwambia Oliver kuzungumza na Hiram Page. Oliver alimwambia kwamba ufunuo aliopokea kupitia jiwe haukutoka kwa Mungu.

Picha
Hiram Page akitafakari

Oliver alisema kwamba Shetani alikuwa amemdanganya Hiram Page. Hiram alimsikiliza Oliver na alitubu.

Picha
Joseph akiwa ameshikilia maandiko

Leo ni Rais wa Kanisa pekee ndiye anayepokea ufunuo kwa ajili ya Kanisa lote. Yeye ni nabii wa Mungu. Waumini wa Kanisa wanapaswa kumtii nabii.

Chapisha