Scripture Stories
Sura ya 32: Kanisa la Yesu Kristo katika Kirtland: 1833–1834


Sura ya 32

Kanisa la Yesu Kristo katika Kirtland

1833–1834

Picha
nyumba ya majira ya baridi
Picha
Joseph Smith na washauri wake

Bwana alisema ya kwamba Joseph Smith anapaswa kuwa na wanaume wa kumsaidia kuongoza Kanisa. Wanaume hawa wangekuwa washauri wa Joseph. Bwana alifunua kuwa Sidney Rigdon na Frederick G. Williams wanapaswa kuwa washauri hawa.

Picha
Joseph akiwatawaza washauri wake

Mnamo Machi 1833, Joseph Smith aliwatawaza washauri wake katika mkutano mtakatifu huko Kirtland, Ohio. Joseph na washauri wake walikuwa Urais wa Kwanza wa Kanisa.

Picha
nabii wa siku za leo

Leo nabii aliye hai ndiye kiongozi wa Kanisa. Yeye na washauri wake ndio Urais wa Kwanza wa Kanisa.

Picha
Watakatifu wakijenga Hekalu la Kirtland

Yesu alimwambia Joseph Smith kwamba Watakatifu wanapaswa kujenga majengo mengi ya Kanisa. Jengo muhimu zaidi lingekuwa hekalu katika Kirtland. Watakatifu pia walihitajika kujenga kiwanda cha uchapishaji na mahali pa Urais wa Kwanza kufanya kazi.

Picha
Watakatifu wakiwekea viunzi Hekalu la Kirtland

Watakatifu walimtii Bwana na kuanza kujenga Hekalu la Kirtland. Ilikuwa kazi ngumu, na Watakatifu wote walihitajika kusaidia.

Picha
patriaki wa kanisa akitoa baraka

Kadiri watu zaidi walivyojiunga na Kanisa, Yesu alimwambia Joseph Smith kuchagua viongozi zaidi. Alisema baba yake Joseph alipaswa kuwa patriaki wa Kanisa. Patriaki hutoa baraka maalum kwa Watakatifu. Leo kuna mapatriaki katika vigingi vingi vya Kanisa.

Picha
Joseph anakutana na baraza kuu

Yesu pia alimwambia Joseph kuchagua wanaume kumi na wawili kutumikia katika baraza kuu. Wajumbe wa baraza kuu wanashikilia ofisi ya kuhani mkuu katika Ukuhani wa Melkizedeki. Mojawapo ya kazi zao ni kusaidia kutatua matatizo yanayoweza kutokea katika Kanisa.

Picha
Watakatifu wanakusanyika

Mnamo Februari 1834, Joseph Smith alianzisha kigingi cha kwanza cha Kanisa. Kigingi ni waumini wengi wa Kanisa wanaoishi katika eneo moja. Watakatifu wote katika Kirtland walikuwa katika kigingi cha kwanza.

Picha
jengo la Kanisa la siku za leo

Leo Kanisa lina maelfu ya vigingi.

Chapisha