Sehemu za Kujua
- Adam-ondi-Ahman
-
Adam-ondi-Ahman ni mahali katika jimbo la Missouri. Yesu alimtembelea Adamu huko miaka mingi iliyopita.
- Amerika
-
Amerika ni nchi ambapo watu wa Kitabu cha Mormoni waliishi miaka mingi iliyopita.
- Arizona
-
Arizona ni jimbo katika magharibi ya Marekani. Brigham Young aliwatuma Watakatifu kujenga miji katika Arizona.
- California
-
California ni jimbo katika magharibi ya Marekani. Brigham Young aliwatuma Watakatifu kujenga miji katika California.
- Carthage
-
Carthage ni mji katika Illinois. Joseph na Hyrum Smith waliuawa katika jela ya Carthage.
- ufalme wa selestia wa mbinguni
-
Ufalme wa selestia wa mbinguni ni mahali ambapo Baba wa Mbinguni na Yesu wanaishi. Watakatifu wenye haki wataishi huko baada ya kufufuka kwao.
- Colorado
-
Colorado ni jimbo katika magharibi ya Marekani.
- Council Bluffs
-
Council Bluffs ni mji katika uwanda wa Marekani. Unapatikana katika Iowa.
- Misri
-
Misri ni nchi ambayo Ibrahimu na Musa waliishi miaka mingi iliyopita.
- Far West
-
Far West ulikuwa mji katika jimbo la Missouri. Watakatifu waliishi katika Far West kwa muda.
- Fayette
-
Fayette ni mji katika jimbo la New York. Joseph Smith alianzisha Kanisa huko Fayette.
- Bustani ya Gethsemane
-
Bustani ya Gethsemane ipo karibu na Yerusalemu. Yesu aliteswa na kumwaga damu kwa ajili yetu katika Bustani ya Gethsemane.
- Bonde Kuu la Salt Lake
-
Bonde Kuu la Salt Lake lipo magharibi ya Marekani.
- Harmony
-
Harmony ni mji katika Pennsylvania ambapo Joseph Smith aliishi.
- Haun’s Mill
-
Haun’s Mill ulikuwa mji katika Missouri. Genge la watu wenye fujo liliwaua Watakatifu wengi katika Haun’s Mill.
- mbinguni
-
Mbinguni ni mahali ambapo Baba wa Mbinguni na Yesu wanaishi. Tuliishi mbinguni kabla ya kuja duniani.
- Kilima Kumora
-
Kilima Kumora kilikuwa karibu na nyumba ya Joseph Smith huko New York. Mabamba ya dhahabu yalizikwa katika Kilima Kumora.
- Idaho
-
Idaho ni jimbo katika magharibi ya Marekani. Brigham Young aliwatuma Watakatifu kujenga miji katika Idaho.
- Illinois
-
Illinois ni jimbo katika magharibi ya kati ya Marekani. Nauvoo na Carthage ni miji katika Illinois.
- Independence
-
Independence ni mji katika Jackson County, Missouri. Yesu alisema kuwa mji wa Sayuni utajengwa karibu na Independence.
- Jackson County
-
Jackson County ipo Missouri. Magenge ya watu wenye fujo yalifanya Watakatifu waondoke Jackson County.
- Yerusalemu
-
Yerusalemu ni mji katika Israeli. Yesu atakwenda Yerusalemu wakati atakapokuja tena duniani.
- Kirtland
-
Kirtland ni mji katika Ohio. Watakatifu wa mwanzo waliishi Kirtland kwa miaka kadhaa na kujenga hekalu huko.
- Liberty
-
Liberty ni mji katika Missouri. Joseph Smith alikuwa katika Jela ya Liberty kwa miezi kadhaa.
- Mto Mississippi
-
Sehemu ya Mto Mississippi ipo karibu na mji wa Nauvoo. Watakatifu walivuka mto Mississippi wakati walipoondoka Nauvoo.
- Missouri
-
Missouri ni jimbo katika magharibi ya kati ya Marekani. Independence ni mji katika Missouri.
- Nauvoo
-
Nauvoo ni mji katika Illinois. Watakatifu waliishi Nauvoo na walijenga hekalu huko.
- New York
-
New York ni jimbo katika mashariki ya Marekani. Kilima Kumora kipo New York. Palmyra na Fayette ni miji katika New York.
- Ohio
-
Ohio ni jimbo katika magharibi ya kati ya Marekani. Kirtland ni mji katika Ohio.
- Bahari ya Pasifiki
-
Bahari ya Pasifiki iko upande wa magharibi mwa Marekani. Kikosi cha Mormoni kiliandamana kuelekea Bahari ya Pasifiki.
- Palmyra
-
Palmyra ni mji katika New York ambapo familia ya Joseph Smith iliishi kwa miaka mingi.
- Pennsylvania
-
Pennsylvania ni jimbo katika mashariki ya Marekani. Familia ya Emma Smith iliishi Pennsylvania.
- Pueblo
-
Pueblo ni mji katika Colorado. Wanaume katika Kikosi cha Mormoni waliacha familia zao huko Pueblo.
- Quincy
-
Quincy ni mji katika Illinois.
- Milima ya Miamba
-
Milima ya Miamba inapatikana katika sehemu ya magharibi ya Marekani. Waanzilishi walivuka Milima ya Miamba na kwenda katika Bonde Kuu la Salt Lake.
- Mji wa Salt Lake
-
Waanzilishi walijenga Mji wa Salt Lake. Unapatikana katika Bonde Kuu la Salt Lake.
- ufalme wa telestia wa mbinguni
-
Watu ambao si wema duniani wataishi katika ufalme wa telestia wa mbinguni baada ya kufufuka.
- ufalme wa terestria wa mbinguni
-
Watu ambao ni wema lakini hawatii amri zote za Mungu duniani wataishi katika ufalme wa terestria wa mbinguni baada kufufuka.
- Marekani
-
Marekani ni nchi katika Amerika ya Kaskazini. Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za Mwisho lilirejeshwa huko Marekani.
- Utah
-
Utah ni jimbo katika magharibi ya Marekani. Mji wa Salt Lake upo Utah.
- Vermont
-
Vermont ni jimbo katika mashariki ya Marekani. Joseph Smith alizaliwa Vermont.
- winter quarters
-
winter quarters ulikuwa mji katika uwanda wa Marekani.
- Wyoming
-
Wyoming ni jimbo katika magharibi ya Marekani. Brigham Young aliwatuma Watakatifu kujenga miji katika Wyoming.
- Sayuni
-
Sayuni ulikuwa ni mji ambao Henoko alijenga. Siku moja kutakuwa na mji mwingine utakaoitwa Sayuni. Utakuwa katika Jackson County, Missouri.