Scripture Stories
Maneno ya Kufahamu


Maneno ya Kufahamu

asiliwa

Joseph na Emma Smith waliasili watoto mapacha. Hii inamaanisha Joseph na Emma waliwafanya watoto mapacha kuwa sehemu ya familia yao.

kileo

Kileo si kizuri kwetu kunywa. Bia na mvinyo zina kileo ndani yake.

mababu

Mababu zetu ni watu katika familia yetu ambao waliishi kabla yetu.

malaika

Malaika ni mmoja wa wasaidizi wa Mungu. Malaika Moroni alizungumza na Joseph Smith.

Picha
malaika
Mtume

Mtume ni kiongozi katika Kanisa la Yesu Kristo. Yesu alimwambia Joseph Smith kuwa Alitaka Mitume. Kumi na Wawili.

kukamatwa

Askari walimkamata Joseph Smith Hii inamaanisha askari walimkamata na kumweka jela.

kushambuliwa

Genge la watu wenye fujo liliwashambulia Watakatifu. Hii inamaanisha genge hilo lilianza kuwapiga Watakatifu.

kisima cha maji ya ubatizo

Kuna visima vya maji ya ubatizo katika makanisa na mahekalu. Watu wanabatizwa katika kisima cha maji ya ubatizo.

kubatizwa

Tunapojiunga na Kanisa, tunabatizwa. Tunawekwa chini ndani ya maji na kuinuliwa tena.

nzuri

Wakati kitu kinapokuwa kizuri, tunapenda kukiangalia. Bustani ni nzuri. Hekalu ni zuri.

amini

Kuamini inamaanisha kufikiri kitu ni cha kweli. Watu wengi wanaamini injili ya Yesu Kristo.

askofu

Askofu ni kiongozi wa kata.

kulaumiwa

Watu walimlaumu Joseph Smith kwa sababu ya matatizo. Hii inamaanisha kwamba watu walisema Joseph Smith alisababisha matatizo yatokee.

azima

Wakati tunapoazima kitu, tunamwuliza mtu kama tunaweza kukitumia. Ikiwa mtu anaazima farasi wa rafiki yake, anamwuliza rafiki yake kama anaweza kumtumia. Baada ya mtu kumtumia farasi huyo, anamrudisha kwa rafiki.

kujigamba

Walinzi wa jela walijigamba kwa kile walichokuwa wamefanya. Hii inamaanisha walikuwa na furaha kuhusu hilo na kuwaambia wengine kuhusu hilo.

daraja

Waanzilishi walivuka mto juu ya daraja.

tarumbeta ndogo

Tarumbeta ndogo ni aina ya pembe.

Picha
tarumbeta ndogo
zikwa

Moroni alizika mabamba ya dhahabu. Aliyaweka katika sanduku la jiwe chini ya ardhi na kuyafunika.

kapteni

Kapteni ni kiongozi. Kapteni Allen alikuwa kiongozi wa askari.

kamatwa

Askari walimkamata Joseph Smith. Hii inamaanisha askari walimshika Joseph Smith na hawakumwachilia aende.

chaguzi

Baba wa Mbinguni anaturuhusu tufanye chaguzi. Hii inamaanisha Baba wa Mbinguni anaturuhusu tuamue kile tutakachofanya.

chagua

Mungu huturuhusu kuchagua kuwa wema au waovu. Tunawachagua watu kuwa viongozi. Mungu alimchagua Brigham Young kuwaongoza Watakatifu.

amri

Watu wema hutii amri za Mungu. Watu wema hufanya kile Mungu anachotaka wafanye.

mkutano

Mkutano ni mkusanyiko mkubwa. Waumini wengi wa Kanisa wanakwenda kwenye mkutano.

washauri

Washauri ni watu ambao humsaidia kiongozi. Nabii wa Kanisa ana washauri.

agano

Agano ni ahadi. Tunapofanya agano na Mungu, tunamwahidi kwamba tutafanya kitu fulani.

kuumbwa

Yesu Kristo aliumba dunia. Hii inamaanisha kwamba Yesu Kristo alitengeneza dunia.

mazao

waanzilishi walipanda mazao. Mazao ni pamoja na mahindi, viazi, ngano, na vitu vingine.

sulubiwa

Yesu alisulubiwa. Hii ina maanisha Yeye alipigiliwa msalabani kwa misumari na kuachwa hapo mpaka alipokufa.

Picha
Yesu alisulubiwa
bwawa

Watakatifu walijenga bwawa kwenye mto. Bwawa linayazuia maji yasiendelee kwenda.

Picha
bwawa
mashemasi

Wavulana wanaweza kuwa mashemasi wanapokuwa na umri wa miaka 12. Mashemasi wanaweza kupitisha sakramenti.

aliamua

Emma na Joseph walijiuliza ikiwa waende Pennsylvania au wabakie New York. Waliamua kwenda Pennsylvania.

weka wakfu

Wakati tunapoweka wakfu kitu, tunakibariki ili kitumike kwa ajili ya kazi ya Mungu. Watakatifu waliweka wakfu hekalu.

haribu

Kuharibu inamaanisha kubomoa, kuvunja, kuchoma, au kuua. Magenge ya watu wenye fujo yaliharibu hekalu.

mwanafunzi

Mwanafunzi ni mtu anayemfuata Yesu na kujaribu kuwa kama Yeye.

pata

Kupata inamaanisha kupata kitu kwa kukifanyia kazi.

wazee

Wazee ni wanaume ambao wana ukuhani.

endaumenti

Endaumenti ni ahadi maalum au zawadi kutoka kwa Mungu .

adui

Adui ni mtu ambaye anamchukia mtu mwingine. Maadui wa Joseph Smith walijaribu kumuua.

toroka

Kutoroka inamaanisha kwenda mbali na mtu au kitu. Joseph Smith alilitoroka genge la watu wenye fujo.

uovu

Uovu ni kitu kibaya sana. Shetani ni roho mwovu.

roho za waovu

Roho Waovu ni roho wabaya Roho Waovu humfuata Shetani

waliotengwa

Waumini wa Kanisa wanaofanya mambo mabaya wanaweza kutengwa. Wao sio tena waumini wa Kanisa.

imani

Kuwa na imani ni kutumainia mambo yasiyoonekana ambayo ni ya kweli. Tuna imani katika Yesu Kristo. Hii inamaanisha tunaamini katika Yeye na kumtii Yeye.

mfungo

Kufunga ni kushinda bila chakula au maji.

milele

Milele inamaanisha daima. Tunaweza kuishi na Baba wa Mbinguni milele ikiwa tutatii amri Zake.

samehe

Kusamehe inamaanisha kusahau mambo mabaya ambayo mtu amefanya. Mungu atatusamehe ikiwa tutahuzunishwa na mambo tuliyoyafanya na kujaribu kutoyafanya tena.

kusanyika

Kukusanyika kunamaanisha kuja pamoja katika sehemu moja. Joseph Smith aliwaambia Watakatifu wakusanyike Missouri.

vipawa

Vipawa ni vitu wanavyopewa watu. Roho Mtakatifu hutoa vipawa vya kiroho kwa watu ambao ni waadilifu.

injili

Injili ya Yesu Kristo ni mpango wa wokovu. Inajumuisha mafundisho yote, ibada, na mamlaka kwa ajili yetu kurudi kuishi na Baba wa Mbinguni.

gavana

Gavana ni kiongozi wa jimbo.

ponya

Kuponya inamaanisha kuwafanya wagonjwa wapate nafuu. Newel K. Whitney alimbariki Joseph Smith, na Joseph aliponywa,

mwaminifu

Watu ambao ni waaminifu hawasemi uongo. Watuwaaminifu hawachukui vitu ambavyo si mali yao.

jela

Wanaume waliwekwa jela. Hii inamaanisha walifungiwa ndani ili wasiweze kutoroka.

Picha
jela
kujiunga

Watu walijiunga na Kanisa. Hii inamaanisha kuwa watu walibatizwa na kuwa waumini wa Kanisa.

lugha

Maneno tunayotumia kuandika au kuzungumza na watu wengine yanaitwa lugha.

ongoza

Kuongoza watu kunamaanisha kuonyesha au kuwaambia cha kufanya. Nabii huongoza Kanisa

funga ndoa

Joseph na Emma walifunga ndoa. Hii inamaanisha Joseph alikuwa mume wa Emma, na Emma alikuwa mke wa Joseph.

misheni

Mtume alikwenda misheni. Hii inamaanisha alikwenda kuwaambia watu kuhusu Injili ya Yesu Kristo.

mmisionari

Mmisionari ni mtu ambaye anaenda misheni.

tii

Kutii humaanisha kufanya kile tulichoambiwa tufanye. Tunapaswa kutii amri za Mungu.

bahari

Bahari ni mkusanyiko mkubwa sana wa maji ya chumvi.

kutawazwa

Kutawazwa inamaanisha kupewa ukuhani. Joseph Smith alimtawaza mwanamume. Hii inamaanisha Joseph Smith alimpa mwanamume ukuhani.

maksai

Maksai ni wanyama.

Picha
maksai
patriaki

Patriaki hutoa baraka maalum kwa watu. Baba yake Joseph Smith alikuwa patriaki.

sumu

Sumu ni kitu ambacho kinaweza kuua watu kama wataila au kuinywa. Genge la watu wenye fujo lilijaribu kumfanya Joseph Smith anywe sumu.

omba

Kuomba inamaanisha kuzungumza na Baba wa Mbinguni.

alihubiri

Joseph Smith aliwahubiria watu. Hii inamaanisha aliwafundisha watu kuhusu Injili.

urais

Urais wa Kanisa ni rais na washauri wake.

rais

Rais ni kiongozi.

ukuhani

Ukuhani ni uwezo wa Mungu.

makuhani

Makuhani wana ukuhani. Makuhani ni watu ambao husaidia katika Kanisa.

mpiga chapa

Mpiga chapa ni mtu ambaye anachapisha vitabu.

gereza

Gereza ni mahali ambapo watu wamewekwa na hawawezi kutoka nje. Gereza ni kama jela.

nabii

Nabii huwaambia watu kile ambacho Mungu anataka wajue. Joseph Smith alikuwa nabii.

linda

Wanaume walikuwa na bunduki ili kuwalinda watu. Hii inamaanisha wanaume walikuwa na bunduki ili kuwaweka watu salama. Bwana alimlinda Joseph Smith. Hii inamaanisha Bwana alimweka Joseph Smith salama.

kware

Kware ni ndege.

Picha
kware
tubu

Kama tunatenda jambo baya, tunapaswa kutubu. Hii inamaanisha tunahuzunika na kujaribu kutofanya jambo baya tena.

kufufuka

Yesu Kristo alifufuka. Hii inamaanisha kwamba baada ya Yeye kufa, Alifanywa hai tena. Watu wote watafufuka baada ya kufa.

ufunuo

Mawasiliano kutoka kwa Mungu kwenda kwa watoto wake duniani yanaitwa ufunuo. Joseph Smith alipokea ufunuo kuhusu hekalu.

uadilifu

Watuwaadilifu hufanya kile kilicho sahihi. Hii inamaanisha wao hutii amri za Mungu.

Sabato

Sabato ni siku ambayo sisi huenda kanisani. Hatupaswi kufanya kazi siku ya Sabato. Jumapili ni siku ya Sabato.

sakramenti

Tunapokea sakramenti kumkumbuka Yesu.

Picha
trei ya sakramenti
takatifu

Hekalu ni jengo takatifu. Hekalu ni mali ya Mungu.

Mtakatifu

Mtakatifu ni muumini wa Kanisa la Yesu Kristo.

okoa

Yesu alikufa ili kutuokoa sisi. Hii inamaanisha Yesu alikufa ili sisi tuweze kurudi kuishi na Baba wa Mbinguni.

maandiko

Maandiko ni vitabu vinavyotuambia kuhusu Mungu. Biblia, Kitabu cha Mormoni, Mafundisho na Maagano, na Lulu ya Thamani Kuu ni maandiko ya Kanisa.

shiriki

Kushiriki maana yake ni kutoa sehemu ya kitu tulichonacho na kumpa mwingine.

askari

Askari wanapigana katika jeshi.

roho

Roho hana mwili wa nyama na mifupa.

iba

Kuiba inamaanisha kuchukua kitu kisicho chako. Magenge ya watu wenye fujo yaliiba mifugo ya Watakatifu. Hii inamaanisha magenge ya watu wenye fujo yalichukua mifugo.

teseka

Tunateseka tunapoumia. Joseph Smith na marafiki zake waliteseka jela.

apa

Kuapa maana yake ni kusema maneno mabaya.

aliapa

Walinzi wa jela waliapa. Walinzi wa jela walisema maneno mabaya.

lami

Lami inanata na ni nyeusi.

hekalu

Hekalu ni nyumba ya Mungu.

jaribu

Shetani anajaribu kutupa majaribu sisi. Hii inamaanisha anajaribu kutufanya sisi tufanye mambo ambayo ni mabaya.

zaka

zaka ni pesa tunayotoa kwa Mungu.

tumbaku

Tumbaku ni kitu kisichofaa kwetu. Baadhi ya watu huvuta na kutafuna tumbaku.

iliyotafsiriwa

Joseph Smith alitafsiri Kitabu cha Mormoni katika lugha ya Kiingereza.

ukweli

Yesu anafundisha watu ukweli. Hii inamaanisha Yesu anafundisha watu kile kilicho sahihi.

ushuhuda

ushuhuda ni hisia kwamba injili ni ya kweli.

watega wanyama

Watega wanyama ni watu wanaowakamata wanyama wamwituni Wao huuza manyoya ya wanyama.

ono

Ono ni kitu ambacho Mungu huturuhusu kuona. Joseph Smith alimwona Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo katika ono.

mashahidi

Mashahidi huona kitu na kuwaambia wengine kuhusu kitu hicho. Mashahidi waliona mabamba ya dhahabu na kuwaambia wengine kuwa mabamba yalikuwa halisi.

abudu

Kuabudu humaanisha kupenda na kutii. Shetani alitaka Musa amwabudu yeye. Tunapaswa kumwabudu Mungu.

jeraha

Jeraha ni sehemu katika mwili wa mtu iliyoumizwa au kukatwa.

Chapisha