Maneno ya Kufahamu
- asiliwa
-
Joseph na Emma Smith waliasili watoto mapacha. Hii inamaanisha Joseph na Emma waliwafanya watoto mapacha kuwa sehemu ya familia yao.
- kileo
-
Kileo si kizuri kwetu kunywa. Bia na mvinyo zina kileo ndani yake.
- mababu
-
Mababu zetu ni watu katika familia yetu ambao waliishi kabla yetu.
- malaika
-
Malaika ni mmoja wa wasaidizi wa Mungu. Malaika Moroni alizungumza na Joseph Smith.
Pichamalaika - Mtume
-
Mtume ni kiongozi katika Kanisa la Yesu Kristo. Yesu alimwambia Joseph Smith kuwa Alitaka Mitume. Kumi na Wawili.
- kukamatwa
-
Askari walimkamata Joseph Smith Hii inamaanisha askari walimkamata na kumweka jela.
- kushambuliwa
-
Genge la watu wenye fujo liliwashambulia Watakatifu. Hii inamaanisha genge hilo lilianza kuwapiga Watakatifu.
- kisima cha maji ya ubatizo
-
Kuna visima vya maji ya ubatizo katika makanisa na mahekalu. Watu wanabatizwa katika kisima cha maji ya ubatizo.
- kubatizwa
-
Tunapojiunga na Kanisa, tunabatizwa. Tunawekwa chini ndani ya maji na kuinuliwa tena.
- nzuri
-
Wakati kitu kinapokuwa kizuri, tunapenda kukiangalia. Bustani ni nzuri. Hekalu ni zuri.
- amini
-
Kuamini inamaanisha kufikiri kitu ni cha kweli. Watu wengi wanaamini injili ya Yesu Kristo.
- askofu
-
Askofu ni kiongozi wa kata.
- kulaumiwa
-
Watu walimlaumu Joseph Smith kwa sababu ya matatizo. Hii inamaanisha kwamba watu walisema Joseph Smith alisababisha matatizo yatokee.
- azima
-
Wakati tunapoazima kitu, tunamwuliza mtu kama tunaweza kukitumia. Ikiwa mtu anaazima farasi wa rafiki yake, anamwuliza rafiki yake kama anaweza kumtumia. Baada ya mtu kumtumia farasi huyo, anamrudisha kwa rafiki.
- kujigamba
-
Walinzi wa jela walijigamba kwa kile walichokuwa wamefanya. Hii inamaanisha walikuwa na furaha kuhusu hilo na kuwaambia wengine kuhusu hilo.
- daraja
-
Waanzilishi walivuka mto juu ya daraja.
- tarumbeta ndogo
-
Tarumbeta ndogo ni aina ya pembe.
Pichatarumbeta ndogo - zikwa
-
Moroni alizika mabamba ya dhahabu. Aliyaweka katika sanduku la jiwe chini ya ardhi na kuyafunika.
- kapteni
-
Kapteni ni kiongozi. Kapteni Allen alikuwa kiongozi wa askari.
- kamatwa
-
Askari walimkamata Joseph Smith. Hii inamaanisha askari walimshika Joseph Smith na hawakumwachilia aende.
- chaguzi
-
Baba wa Mbinguni anaturuhusu tufanye chaguzi. Hii inamaanisha Baba wa Mbinguni anaturuhusu tuamue kile tutakachofanya.
- chagua
-
Mungu huturuhusu kuchagua kuwa wema au waovu. Tunawachagua watu kuwa viongozi. Mungu alimchagua Brigham Young kuwaongoza Watakatifu.
- amri
-
Watu wema hutii amri za Mungu. Watu wema hufanya kile Mungu anachotaka wafanye.
- mkutano
-
Mkutano ni mkusanyiko mkubwa. Waumini wengi wa Kanisa wanakwenda kwenye mkutano.
- washauri
-
Washauri ni watu ambao humsaidia kiongozi. Nabii wa Kanisa ana washauri.
- agano
-
Agano ni ahadi. Tunapofanya agano na Mungu, tunamwahidi kwamba tutafanya kitu fulani.
- kuumbwa
-
Yesu Kristo aliumba dunia. Hii inamaanisha kwamba Yesu Kristo alitengeneza dunia.
- mazao
-
waanzilishi walipanda mazao. Mazao ni pamoja na mahindi, viazi, ngano, na vitu vingine.
- sulubiwa
-
Yesu alisulubiwa. Hii ina maanisha Yeye alipigiliwa msalabani kwa misumari na kuachwa hapo mpaka alipokufa.
PichaYesu alisulubiwa - bwawa
-
Watakatifu walijenga bwawa kwenye mto. Bwawa linayazuia maji yasiendelee kwenda.
Pichabwawa - mashemasi
-
Wavulana wanaweza kuwa mashemasi wanapokuwa na umri wa miaka 12. Mashemasi wanaweza kupitisha sakramenti.
- aliamua
-
Emma na Joseph walijiuliza ikiwa waende Pennsylvania au wabakie New York. Waliamua kwenda Pennsylvania.
- weka wakfu
-
Wakati tunapoweka wakfu kitu, tunakibariki ili kitumike kwa ajili ya kazi ya Mungu. Watakatifu waliweka wakfu hekalu.
- haribu
-
Kuharibu inamaanisha kubomoa, kuvunja, kuchoma, au kuua. Magenge ya watu wenye fujo yaliharibu hekalu.
- mwanafunzi
-
Mwanafunzi ni mtu anayemfuata Yesu na kujaribu kuwa kama Yeye.
- pata
-
Kupata inamaanisha kupata kitu kwa kukifanyia kazi.
- wazee
-
Wazee ni wanaume ambao wana ukuhani.
- endaumenti
-
Endaumenti ni ahadi maalum au zawadi kutoka kwa Mungu .
- adui
-
Adui ni mtu ambaye anamchukia mtu mwingine. Maadui wa Joseph Smith walijaribu kumuua.
- toroka
-
Kutoroka inamaanisha kwenda mbali na mtu au kitu. Joseph Smith alilitoroka genge la watu wenye fujo.
- uovu
-
Uovu ni kitu kibaya sana. Shetani ni roho mwovu.
- roho za waovu
-
Roho Waovu ni roho wabaya Roho Waovu humfuata Shetani
- waliotengwa
-
Waumini wa Kanisa wanaofanya mambo mabaya wanaweza kutengwa. Wao sio tena waumini wa Kanisa.
- imani
-
Kuwa na imani ni kutumainia mambo yasiyoonekana ambayo ni ya kweli. Tuna imani katika Yesu Kristo. Hii inamaanisha tunaamini katika Yeye na kumtii Yeye.
- mfungo
-
Kufunga ni kushinda bila chakula au maji.
- milele
-
Milele inamaanisha daima. Tunaweza kuishi na Baba wa Mbinguni milele ikiwa tutatii amri Zake.
- samehe
-
Kusamehe inamaanisha kusahau mambo mabaya ambayo mtu amefanya. Mungu atatusamehe ikiwa tutahuzunishwa na mambo tuliyoyafanya na kujaribu kutoyafanya tena.
- kusanyika
-
Kukusanyika kunamaanisha kuja pamoja katika sehemu moja. Joseph Smith aliwaambia Watakatifu wakusanyike Missouri.
- vipawa
-
Vipawa ni vitu wanavyopewa watu. Roho Mtakatifu hutoa vipawa vya kiroho kwa watu ambao ni waadilifu.
- injili
-
Injili ya Yesu Kristo ni mpango wa wokovu. Inajumuisha mafundisho yote, ibada, na mamlaka kwa ajili yetu kurudi kuishi na Baba wa Mbinguni.
- gavana
-
Gavana ni kiongozi wa jimbo.
- ponya
-
Kuponya inamaanisha kuwafanya wagonjwa wapate nafuu. Newel K. Whitney alimbariki Joseph Smith, na Joseph aliponywa,
- mwaminifu
-
Watu ambao ni waaminifu hawasemi uongo. Watuwaaminifu hawachukui vitu ambavyo si mali yao.
- jela
-
Wanaume waliwekwa jela. Hii inamaanisha walifungiwa ndani ili wasiweze kutoroka.
Pichajela - kujiunga
-
Watu walijiunga na Kanisa. Hii inamaanisha kuwa watu walibatizwa na kuwa waumini wa Kanisa.
- lugha
-
Maneno tunayotumia kuandika au kuzungumza na watu wengine yanaitwa lugha.
- ongoza
-
Kuongoza watu kunamaanisha kuonyesha au kuwaambia cha kufanya. Nabii huongoza Kanisa
- funga ndoa
-
Joseph na Emma walifunga ndoa. Hii inamaanisha Joseph alikuwa mume wa Emma, na Emma alikuwa mke wa Joseph.
- misheni
-
Mtume alikwenda misheni. Hii inamaanisha alikwenda kuwaambia watu kuhusu Injili ya Yesu Kristo.
- mmisionari
-
Mmisionari ni mtu ambaye anaenda misheni.
- tii
-
Kutii humaanisha kufanya kile tulichoambiwa tufanye. Tunapaswa kutii amri za Mungu.
- bahari
-
Bahari ni mkusanyiko mkubwa sana wa maji ya chumvi.
- kutawazwa
-
Kutawazwa inamaanisha kupewa ukuhani. Joseph Smith alimtawaza mwanamume. Hii inamaanisha Joseph Smith alimpa mwanamume ukuhani.
- maksai
-
Maksai ni wanyama.
Pichamaksai - patriaki
-
Patriaki hutoa baraka maalum kwa watu. Baba yake Joseph Smith alikuwa patriaki.
- sumu
-
Sumu ni kitu ambacho kinaweza kuua watu kama wataila au kuinywa. Genge la watu wenye fujo lilijaribu kumfanya Joseph Smith anywe sumu.
- omba
-
Kuomba inamaanisha kuzungumza na Baba wa Mbinguni.
- alihubiri
-
Joseph Smith aliwahubiria watu. Hii inamaanisha aliwafundisha watu kuhusu Injili.
- urais
-
Urais wa Kanisa ni rais na washauri wake.
- rais
-
Rais ni kiongozi.
- ukuhani
-
Ukuhani ni uwezo wa Mungu.
- makuhani
-
Makuhani wana ukuhani. Makuhani ni watu ambao husaidia katika Kanisa.
- mpiga chapa
-
Mpiga chapa ni mtu ambaye anachapisha vitabu.
- gereza
-
Gereza ni mahali ambapo watu wamewekwa na hawawezi kutoka nje. Gereza ni kama jela.
- nabii
-
Nabii huwaambia watu kile ambacho Mungu anataka wajue. Joseph Smith alikuwa nabii.
- linda
-
Wanaume walikuwa na bunduki ili kuwalinda watu. Hii inamaanisha wanaume walikuwa na bunduki ili kuwaweka watu salama. Bwana alimlinda Joseph Smith. Hii inamaanisha Bwana alimweka Joseph Smith salama.
- kware
-
Kware ni ndege.
Pichakware - tubu
-
Kama tunatenda jambo baya, tunapaswa kutubu. Hii inamaanisha tunahuzunika na kujaribu kutofanya jambo baya tena.
- kufufuka
-
Yesu Kristo alifufuka. Hii inamaanisha kwamba baada ya Yeye kufa, Alifanywa hai tena. Watu wote watafufuka baada ya kufa.
- ufunuo
-
Mawasiliano kutoka kwa Mungu kwenda kwa watoto wake duniani yanaitwa ufunuo. Joseph Smith alipokea ufunuo kuhusu hekalu.
- uadilifu
-
Watuwaadilifu hufanya kile kilicho sahihi. Hii inamaanisha wao hutii amri za Mungu.
- Sabato
-
Sabato ni siku ambayo sisi huenda kanisani. Hatupaswi kufanya kazi siku ya Sabato. Jumapili ni siku ya Sabato.
- sakramenti
-
Tunapokea sakramenti kumkumbuka Yesu.
Pichatrei ya sakramenti - takatifu
-
Hekalu ni jengo takatifu. Hekalu ni mali ya Mungu.
- Mtakatifu
-
Mtakatifu ni muumini wa Kanisa la Yesu Kristo.
- okoa
-
Yesu alikufa ili kutuokoa sisi. Hii inamaanisha Yesu alikufa ili sisi tuweze kurudi kuishi na Baba wa Mbinguni.
- maandiko
-
Maandiko ni vitabu vinavyotuambia kuhusu Mungu. Biblia, Kitabu cha Mormoni, Mafundisho na Maagano, na Lulu ya Thamani Kuu ni maandiko ya Kanisa.
- shiriki
-
Kushiriki maana yake ni kutoa sehemu ya kitu tulichonacho na kumpa mwingine.
- askari
-
Askari wanapigana katika jeshi.
- roho
-
Roho hana mwili wa nyama na mifupa.
- iba
-
Kuiba inamaanisha kuchukua kitu kisicho chako. Magenge ya watu wenye fujo yaliiba mifugo ya Watakatifu. Hii inamaanisha magenge ya watu wenye fujo yalichukua mifugo.
- teseka
-
Tunateseka tunapoumia. Joseph Smith na marafiki zake waliteseka jela.
- apa
-
Kuapa maana yake ni kusema maneno mabaya.
- aliapa
-
Walinzi wa jela waliapa. Walinzi wa jela walisema maneno mabaya.
- lami
-
Lami inanata na ni nyeusi.
- hekalu
-
Hekalu ni nyumba ya Mungu.
- jaribu
-
Shetani anajaribu kutupa majaribu sisi. Hii inamaanisha anajaribu kutufanya sisi tufanye mambo ambayo ni mabaya.
- zaka
-
zaka ni pesa tunayotoa kwa Mungu.
- tumbaku
-
Tumbaku ni kitu kisichofaa kwetu. Baadhi ya watu huvuta na kutafuna tumbaku.
- iliyotafsiriwa
-
Joseph Smith alitafsiri Kitabu cha Mormoni katika lugha ya Kiingereza.
- ukweli
-
Yesu anafundisha watu ukweli. Hii inamaanisha Yesu anafundisha watu kile kilicho sahihi.
- ushuhuda
-
ushuhuda ni hisia kwamba injili ni ya kweli.
- watega wanyama
-
Watega wanyama ni watu wanaowakamata wanyama wamwituni Wao huuza manyoya ya wanyama.
- ono
-
Ono ni kitu ambacho Mungu huturuhusu kuona. Joseph Smith alimwona Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo katika ono.
- mashahidi
-
Mashahidi huona kitu na kuwaambia wengine kuhusu kitu hicho. Mashahidi waliona mabamba ya dhahabu na kuwaambia wengine kuwa mabamba yalikuwa halisi.
- abudu
-
Kuabudu humaanisha kupenda na kutii. Shetani alitaka Musa amwabudu yeye. Tunapaswa kumwabudu Mungu.
- jeraha
-
Jeraha ni sehemu katika mwili wa mtu iliyoumizwa au kukatwa.