Scripture Stories
Sura ya 18: Sheria ya Kanisa: Februari 9 1831


Sura ya 18

Sheria ya Kanisa

Februari 9, 1831

Picha
ubatizo
Picha
Joseph akiandika ufunuo

Katika Kirtland, Ohio, Bwana alitoa ufunuo muhimu sana kwa Joseph Smith. Unaitwa sheria ya Kanisa.

Mafundisho na Maagano 42, kichwa cha habari cha sehemu

Picha
mtu akiwa anatawazwa

Bwana alisema Watakatifu wanapaswa kufundisha injili kwa watu wote. Wanaume wanaokwenda misheni wanapaswa kutawazwa kwenye ukuhani na viongozi wa Kanisa.

Picha
wamisionari wakifundisha familia

Wamisionari wawili wanapaswa kufanya kazi kwa pamoja. Wanapaswa kufundisha kutoka kwenye Biblia na Kitabu cha Mormoni. Wanapaswa kuomba ili Roho Mtakatifu awe pamoja nao. Roho Mtakatifu angewaambia cha kufundisha.

Picha
wamisionari wakimbatiza mvulana

Wamisionari wanapaswa kuwabatiza watu wanaoiamini injili.

Picha
waumini wa Kanisa wakisalimiana

Bwana alisema waumini wa Kanisa wanapaswa kutii Amri Kumi. Hawapaswi kuua. Hawapaswi kusema uongo. Hawapaswi kusema mambo mabaya juu ya watu wengine. Hawapaswi kufanya mambo mengine mabaya.

Picha
Watakatifu wakigawiana chakula

Watakatifu wanapaswa kushiriki kile walichonacho na watu wengine. Kushiriki na wengine ni kama kushiriki na Yesu.

Picha
Watakatifu wakifanya kazi

Yesu aliwapa Watakatifu amri zingine. Hakuna Mtakatifu anayepaswa kufikiri kuwa yeye ni bora kuliko mtu mwingine. Watakatifu wanapaswa kuwa wasafi. Wanapaswa kufanya kazi kwa bidii.

Picha
wazee wakimbariki msichana mgonjwa

Watakatifu wanapaswa kuwahudumia waumini wagonjwa. Wanaume wenye ukuhani wanapaswa kuwabariki wagonjwa. Wale wenye imani wanaweza kuponywa. Hawatakufa kama si wakati wa wao kufa.

Picha
roho ya mwanadamu ikiuacha mwili wake

Watakatifu wenye haki hawapaswi kuwa na hofu ya kufa. Kifo ni cha kupendeza kwa watu wenye haki.

Picha
Joseph akiwapa maelekezo Watakatifu

Yesu alisema Angefunua mambo mengi kwa waumini wenye haki. Mafunuo haya yangeleta furaha. Bwana aliwaambia Watakatifu kutii sheria ya Kanisa.

Chapisha