Sura ya 18
Sheria ya Kanisa
Februari 9, 1831
Katika Kirtland, Ohio, Bwana alitoa ufunuo muhimu sana kwa Joseph Smith. Unaitwa sheria ya Kanisa.
Mafundisho na Maagano 42, kichwa cha habari cha sehemu
Bwana alisema Watakatifu wanapaswa kufundisha injili kwa watu wote. Wanaume wanaokwenda misheni wanapaswa kutawazwa kwenye ukuhani na viongozi wa Kanisa.
Mafundisho na Maagano 42, kichwa cha habari cha sehemu
Wamisionari wawili wanapaswa kufanya kazi kwa pamoja. Wanapaswa kufundisha kutoka kwenye Biblia na Kitabu cha Mormoni. Wanapaswa kuomba ili Roho Mtakatifu awe pamoja nao. Roho Mtakatifu angewaambia cha kufundisha.
Wamisionari wanapaswa kuwabatiza watu wanaoiamini injili.
Bwana alisema waumini wa Kanisa wanapaswa kutii Amri Kumi. Hawapaswi kuua. Hawapaswi kusema uongo. Hawapaswi kusema mambo mabaya juu ya watu wengine. Hawapaswi kufanya mambo mengine mabaya.
Watakatifu wanapaswa kushiriki kile walichonacho na watu wengine. Kushiriki na wengine ni kama kushiriki na Yesu.
Yesu aliwapa Watakatifu amri zingine. Hakuna Mtakatifu anayepaswa kufikiri kuwa yeye ni bora kuliko mtu mwingine. Watakatifu wanapaswa kuwa wasafi. Wanapaswa kufanya kazi kwa bidii.
Watakatifu wanapaswa kuwahudumia waumini wagonjwa. Wanaume wenye ukuhani wanapaswa kuwabariki wagonjwa. Wale wenye imani wanaweza kuponywa. Hawatakufa kama si wakati wa wao kufa.
Watakatifu wenye haki hawapaswi kuwa na hofu ya kufa. Kifo ni cha kupendeza kwa watu wenye haki.
Yesu alisema Angefunua mambo mengi kwa waumini wenye haki. Mafunuo haya yangeleta furaha. Bwana aliwaambia Watakatifu kutii sheria ya Kanisa.