Scripture Stories
Sura ya 27: Nabii Anaendelea na Kazi Yake Licha ya Mateso: Machi 1832


Sura ya 27

Nabii Anaendelea na Kazi Yake Licha ya Mateso

Machi 1832

Picha
gari la kukokotwa na maksai
Picha
Joseph akisoma Biblia

Joseph Smith na Sidney Rigdon waliendelea kufanya marekebisho yenye mwongozo wa kiungu kwenye Biblia. Yesu alimfunulia Joseph Smith masahihisho yaliyopaswa kufanywa, na Sidney Rigdon aliyaandika (ona sura ya 16).

Picha
Joseph akitafsiri Biblia

Joseph Smith hakuelewa baadhi ya sehemu za Biblia. Aliomba kwa ajili ya uelewa, na Bwana alijibu. Mengi ya mafunuo katika Mafundisho na Maagano yalikuja kama majibu ya maswali ambayo Nabii alimwuliza Bwana wakati akitafsiri Biblia (ona, kwa mfano, Mafundisho na Maagano 76, 77, na 113).

Picha
Joseph akiandika mezani

Yesu alikuwa na furaha kwa kazi ya Joseph. Joseph alikuwa nabii mkuu.

Picha
Joseph na Emma Smith wakiwa na mapacha

Wakati huu, Joseph na Emma Smith walikuwa na watoto mapacha ambao waliishi kwa masaa machache tu. Marafiki wa Joseph na Emma pia walikuwa na watoto mapacha. Mama wa mapacha hawa alifariki, na baba yao aliwaruhusu Joseph na Emma kuwaasili.

Picha
genge la watu wenye fujo likimchukua Joseph

Usiku mmoja genge la watu wenye hasira walikwenda nyumbani kwa Joseph. Walivunja mlango na kuingia ndani. Joseph alikuwa amemshikilia mmoja wa watoto wadogo, ambaye alikuwa mgonjwa sana.

Picha
Joseph akiburuzwa nje

Wanaume walimkamata Joseph na kumburuta hadi nje katika usiku wenye baridi. Mtoto alibaki peke yake, na siku tano baadaye alifariki.

Picha
Watu wakijaribu kumuua Joseph

Watu walimsonga Joseph na kujaribu kummwagia sumu katika kinywa chake. Chupa ilivunja moja ya meno yake, na sumu ilimwunguza.

Picha
watu wakimmwagia lami na manyoya Joseph

Watu walirarua mavazi ya Joseph na kupaka lami kwenye ngozi yake. Walifunika lami kwa manyoya na kumpiga.

Picha
Joseph akiwa amwemwagiwa lami na manyoya

Genge liliondoka, wakifikiri Joseph angekufa. Joseph alijaribu kusimama, lakini hakuweza. Alipumzika kwa muda, kisha akapata nguvu ya kutosha kutambaa kurudi ndani.

Picha
Emma akilia

Marafiki wa Joseph walisafisha lami kutoka kwenye mwili wake. Ilikuwa ni vigumu kuitoa lami. Ngozi yake ilikuwa imeungua na kuvimba.

Picha
Joseph akifundisha

Siku iliyofuata ilikuwa Jumapili. Katika maumivu makali, Joseph alikwenda kanisani na kutoa hotuba. Baadhi ya watu katika genge walikuja kwenye mkutano na walishangaa kumwona Joseph. Nabii hakuwaruhusu kumzuia kufanya kazi ya Bwana.

Chapisha