Scripture Stories
Sura ya 33: Ufunuo kuhusu Yesu Kristo: Mei 1833


Sura ya 33

Ufunuo kuhusu Yesu Kristo

Mei 1833

Picha
nyumba ya majira ya baridi
Picha
Joseph anapokea ufunuo

Katika mojawapo ya mafunuo kwa Nabii Joseph Smith, Yesu alielezea kuhusu Yeye mwenyewe. Alisema watu wanaweza kuuona uso Wake na kumjua Yeye kama watatii amri Zake na kuomba.

Picha
Yesu Kristo

Yesu alisema Yeye ni Nuru ya Ulimwengu. Anatuonyesha njia sahihi ya kuishi.

Picha
Yesu akiumba dunia

Yesu aliishi na Baba wa Mbinguni kabla ya dunia kutengenezwa. Yesu aliumba dunia na vitu vyote vilivyo ndani yake.

Picha
kijana Joseph akiomba

Yesu hakuwa kama Baba yake wa Mbinguni mwanzoni. Hakujua mambo yote ambayo Baba Yake alijua, na hakuwa na nguvu zote na utukufu ambao Baba Yake alikuwa nao. Yesu alijaribu sana kuwa kama Baba Yake. Hatua kwa hatua Yeye alipokea nguvu na utukufu wa Baba Yake.

Picha
Joseph akimwona Yesu mbinguni

Yesu alisema tunapaswa kutii amri za Mungu. Kadiri tunavyotii, tunaweza kuja kujua mambo yote. Tunaweza pia kuwa kama Mungu na kupokea utimilifu wa baraka Zake.

Picha
Joseph akiifundisha familia yake

Yesu alisema Shetani hataki watu wajue ukweli na kuwa kama Mungu. Yesu alimwambia Joseph aifundishe familia yake ukweli.

Picha
Sidney Rigdon akiifundisha familia yake

Yesu pia alimwambia Frederick G. Williams na Sidney Rigdon kufundisha familia zao kuhusu ukweli na kutii amri. Hapo Shetani asingeweza kuwa na nguvu juu yao.

Chapisha