Mafundisho na Maagano 2021
Agosti 30–Septemba 5. Mafundisho na Maagano 94–97: “Kwa ajili ya Wokovu wa Sayuni”


“Agosti 30–Septemba 5. Mafundisho na Maagano 94–97: ‘Kwa ajili ya Wokovu wa Sayuni,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Agosti 30–Septemba 5. Mafundisho na Maagano 94–97,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2021

Picha
Hekalu la Kirtland

Hekalu la Kirtland, na Al Rounds

Agosti 30–Septemba 5

Mafundisho na Maagano 94–97

“Kwa ajili ya Wokovu wa Sayuni”

Tafuta mwongozo wa kiungu ili kujua ni kanuni zipi kutoka sehemu ya 94–97 zisisitizwe wakati ukifundisha. Unaweza kutohoa mawazo ya shughuli kwa watoto wadogo wakati unapowafundisha watoto wakubwa, na kinyume chake.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waoneshe watoto picha ya hekalu, na waalike kushiriki kile wanachojua kuhusu hekalu. Wangeweza pia kuongelea juu ya namna wanavyohisi wakati wanapoliona hekalu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mafundisho na Maagano 95:8; 97:15–16.

Hekalu ni nyumba ya Bwana.

Hata watoto huko Kirtland walisaidia, katika njia ndogo lakini zenye maana, ili kulijenga Hekalu la Kirtland. Wasaidie watoto unaowafundisha kuimarisha upendo wao kwa ajili ya nyumba takatifu ya Bwana.

Shughuli Yamkini

  • Onesha picha ya Hekalu la Kirtland (ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia.). Tumia vifungu vya maneno kutoka Mafundisho na Maagano 95:8 kuwafundisha watoto juu ya amri ya Bwana ya kujenga hekalu hili. Acha watoto wafanye zamu kushikilia picha na kusema “Hekalu ni Nyumba ya Bwana.”

    Picha
    Hekalu la Kirtland

    Watakatifu walijenga hekalu ili kuhisi wako karibu zaidi na Mungu?

  • Waambie watoto kwamba juu ya kila hekalu pameandikwa “Utakatifu kwa Bwana. Nyumba ya Bwana.” Kama inawezekana, waoneshe picha ya maneno haya juu ya hekalu. Je ni kwa nini hekaluni ni mahali maalumu? Soma vifungu vya maneno kutoka Mafundisho na Maagano 97:15–16 ambavyo vinafundisha kuhusu hekalu kuwa ni nyumba ya Bwana, na shiriki hisia zako juu ya hekalu.

  • Waalike watoto kujifanya wanasaidia kujenga hekalu (kukata miti, kupigilia misumari, kupaka rangi kuta, na kadhalika). Elezea jinsi hekalu lilivyo muhimu kwa Bwana, namna gani Watakatifu walivyofanya kazi kwa bidii ili kujenga Hekalu la Kirtland, na kwa kiasi gani walijitolea dhabihu kwa ajili ya hekalu hilo (ona Watakatifu, 1:210).

  • Imbeni pamoja wimbo ili kuwasaidia watoto kuhisi unyenyekevu kwa ajili ya nyumba ya Bwana, kama vile “I Love to See the Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 95). Acha watoto washiriki hisia zao kuhusu hekalu.

Mafundisho na Maagano 97:8

Naweza kuwa mwaminifu.

Katika Mafundisho na Maagano 97:8, Bwana anatambulisha uaminifu kama moja ya sifa za wale ambao “wanakubalika kwangu.”

Shughuli Yamkini

  • Waelezee watoto kwamba Mungu alifundisha kwamba tunapokuwa waaminifu, Yeye anatukubali (ona Mafundisho na Maagano 97:8). Shiriki pamoja nao hadithi chache fupi ambazo zinawasaidia wao kuelewa kile inachomaanisha kuwa mwaminifu. Hadithi hizi zinaweza kutokana na maisha yako wewe mwenyewe, kutoka katika maisha ya mtu mwingine unayemfahamu, au kutoka kwenye Friend au Liahona. Wasaidie watoto kusimulia tena hadithi hizo kwako au kushiriki uzoefu wa uaminifu kutoka katika maisha yao.

  • Wasaidie watoto kujifunza aya ya kwanza ya makala ya 13 ya imani: “Tunaamini katika kuwa waaminifu.” Wasaidie watoto kuigiza mifano ya kuwa waaminifu na kutokuwa waaminifu. Kwa mfano, watoto wanaweza kuigiza kuchukua kitu fulani kutoka kwa nduguye na kuwaambia wazazi wao kwamba hawakukichukua. Kisha wasaidie watoto kuigiza onyesho kama hilo ambapo wanasema ukweli kwa wazazi wao. Elezea kwamba kuwa hivyo ndivyo kuwa mwaminifu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mafundisho na Maagano 95:1–3, 8, 11–17; 97:10–17

Hekalu ni nyumba ya Bwana.

Tafakari jinsi unavyoweza kutumia mistari hii kuwasaidia watoto kuelewa jinsi hekalu lilivyo muhimu kwa Bwana—na jinsi linavyopaswa kuwa muhimu kwetu sote.

Shughuli Yamkini

  • Watake watoto kuelezea juu ya wakati ambapo walitakiwa kufanya kitu fulani lakini hawakufanya hivyo mara moja. Msaidie mtoto kusoma Mafundisho na Maagano 95:3, 8, na waulize watoto ni amri gani Bwana alisema Watakatifu walikuwa hawajaitii. Someni pamoja mstari wa 11. Je, Watakatifu walihitaji kufanya nini ili kuweza kujenga hekalu? Tunaweza kujifunza nini kutokana na ahadi ya Bwana kwao?

  • Juu ya kadi, andika kanuni kuhusu hekalu zinazopatikana katika Mafundisho na Maagano 95 na 97, sambamba na marejeleo yanayohusiana, na ziweke kadi ndani ya begi. Kwa mfano: Kujenga mahekalu kunahitaji dhabihu (Mafundisho na Maagano 97:11–12) na ni lazima tuwe wenye kustahili ili kuingia hekaluni (Mafundisho na Maagano 97:15–17). Wagawe watoto katika jozi. Ruhusu kila jozi ichukue kadi moja kutoka katika begi na kisha wafanye kazi pamoja kwa kusoma andiko kwenye kadi hiyo na kuzungumza kuhusu kanuni hiyo ina maana gani kwao. Wasaidie watoto kuelewa kile wanachosoma kadiri inavyohitajika.

  • Mwalike kijana kutoka katika kata au tawi lako ambaye amewahi kuingia hekaluni ili ashiriki uzoefu wake na kuwaambia watoto kile wanachoweza kufanya ili kujiandaa kwa ajili ya kwenda hekaluni.

  • Tumia makala “Your Path to the Temple” (katika Mahekalu ya Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho [toleo maalumu la Ensign au Liahona, Okt. 2010], 72–75) ili kuwasaidia watoto kuelewa kile kinachotendeka ndani ya mahekalu na namna wao wanavyoweza kujiandaa. Fikiria kumpa kila mtoto kipengele cha makala ili asome na kuwaruhusu kuelezea kile wanachojifunza.

  • Onesha video ya “Two Apostles Lead a Virtual Tour of the Rome Italy Temple” (ChurchofJesus Christ.org), na waalike watoto kuelezea jinsi wanavyohisi juu ya kwenda hekaluni siku moja.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu hekalu, kama vile “I Love to See the Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 95). Ni vifungu gani vya maneno katika wimbo huu hutufundisha sisi kwa nini hekalu ni takatifu?

Mafundisho na Maagano 97: 1–2, 8–9, 21

Sayuni ni “walio safi moyoni.”

Wasaidie watoto kuelewa kwamba Sayuni sio mahali tu; pia ni “walio safi moyoni” (Mafundisho na Maagano 97:21).

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wasome Mafundisho na Maagano 97:21, na waulize neno “safi” lina maana gani. Ili kufafanua, waoneshe glasi yenye maji safi, na jadili kwa nini ni muhimu kuwa na maji safi. Ongeza kitu kingine kwenye maji ambacho hufanya maji yasiwe safi (kama vile vumbi au pilipili). Waalike watoto wasome Mafundisho na Maagano 97:21 tena na waweke kidole chao juu ya neno “safi.” Inamaanisha nini kwa mioyo yetu kuwa safi? Wasaidie watoto kuelewa kwamba kuwa safi moyoni hakumaanishi kuwa kamwe hatufanyi makosa. Tunaweza kufanya nini ili kuwa safi zaidi moyoni? Ni jinsi gani Mwokozi anatusaidia sisi?

  • Wasaidie watoto kuchunguza Mafundisho na Maagano 97:1–2, 8–9, 21, wakitafuta maneno au vifungu vya maneno ambavyo vinaeleza jinsi ya kuwa safi moyoni. Waombe watoto wachague neno au kifungu cha maneno, wakiandike kwenye kipande cha karatasi, na kukiweka ndani ya chombo. Toa kipande kimoja kimoja, na waombe watoto kupendekeza mambo wanayoweza kufanya ili kutumia wazo hilo katika maisha yao. Kwa mfano, tunaweza kufanya nini ili “kupata ukweli”, (mstari wa 1) au kuwa “waaminifu” zaidi (mstari wa 8)?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kutumia ukurasa wa shughuli ya wiki hii ili kushiriki na familia zao kile walichojifunza leo kuhusu hekalu.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wahimize watoto kuuliza maswali “Jitahidi kuona maswali ya [watoto] kama fursa, siyo kama usumbufu au vizuizi kwenye somo lako. … Maswali kama haya yanakupa utambuzi muhimu wa kujua kile watoto wanachofikiria, wasiwasi walio nao, na jinsi wanavyoitikia mambo wanayojifunza. Wasaidie kuona kwamba majibu ya maswali yao yanaweza kupatikana katika maandiko na maneno ya manabii walio hai” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26).

Chapisha