Njoo, Unifuate
Aprili 22–28. Mathayo 18: Luka 10: ‘Nifanye Nini Ili Nipate Kuurithi Uzima wa Milele?’


“Aprili 22–28. Mathayo 18: Luka 10: ‘Nifanye Nini Ili Nipate Kuurithi Uzima wa Milele?’“ Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Aprili 22–28. Mathayo 18: Luka 10.“ Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Msamaria Mwema

Msamaria mwema na Dan Burr

Aprili 22–28

Mathayo 18; Luka 10

“Nifanye Nini Ili Nipate Kuurithi Uzima wa Milele?”

Kweli gani katika Mathayo 18 na Luka 10 watoto wanapaswa kujifunza? Sikiliza mnong’ono wa Roho Mtakatifu unaposoma sura hizi. Njoo, Unifuate—Kwa Watu Binafsi na Familia inaweza kukusaidia kuelewa mafundisho, na muhtasari huu unaweza kukupa mawazo ya jinsi ya kufundisha kweli hizi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waombe watoto washiriki jinsi walivyosherehekea Upatanisho wa Yesu Kristo katika Pasaka.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

Mathayo 18:21–35

Ninapaswa kuwasamehe wengine kila siku.

Unaposoma Mathayo 18:21–35, zingatia uzoefu wako katika msamaha na nini watoto wanahitaji kujua kuhusiana na kanuni hii.

Shughuli za Yakini

  • Soma Mathayo 18:21, na waalike watoto kusema “ninakusamehe” mara saba. Uliza, “Je, kusamehe mara saba inatosha?” Soma mstari 22 na eleza kwamba Yesu anatutaka tuchague kusamehe kila mara.

  • Simulia hadithi ya mtumishi asiye na huruma (ona Mathayo 18:23–35). Ikiwa ni lazima, kuelezea kwamba wakati mtu ametenda jambo lisilo zuri kwetu, labda tutajisikia hasira au huzuni mwanzoni. Lakini msamaha unamaanisha tunaweza kuhisi amani tena. (Unaweza kuhisi kusukumwa kuwasaidia watoto kuelewa kwamba kama mtu fulani anawadhuru, wanapaswa kuwaambia wazazi wao au mtu mwingine mzima anayeaminiwa.)

  • Andika nimekusamehe katika ubao, na waambie watoto kwamba maneno haya yanaweza kuwasaidia kugeuza nyakati za huzuni kuwa za furaha. Chora sura yenye huzuni ubaoni, na shiriki baadhi ya mifano ya watoto wakisameheana. Baada ya kila mfano, mwalike mtoto kubadilisha sura yenye huzuni kuwa yenye furaha.

  • Imba pamoja na watoto “Nisaidie, Baba Yangu.” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99. Waombe wasimame wanaposikia neno nisaidie. Toa ushuhuda wako kwamba Baba wa Mbinguni atatusaidia kusamehe wengine.

Luka 10:25–37

Yesu alinifundisha kuwaona watu wote kama majirani zangu na kuwapenda.

Na fumbo la Msamaria mwema ni hadithi ya kukumbukwa inayoweza kuonyesha watoto majirani zetu ni kina nani. Fikiria juu ya njia unaweza kuwahamasisha watoto “kwenda, na kufanya … vivyo hivyo” (Luka 10:37).

Shughuli za Yakini

  • Muulize kila mtoto, “Ni nani jirani yako?” Eleza kwamba Yesu alifundisha kwamba kila atakaye msaada wetu ni jirani yetu pia, hata kama haishi karibu nasi, na tunapaswa kumtendea mtu huyo kwa upendo.

  • Soma Luka 10:25–37 watoto wanapoigiza fumbo la Msamaria mwema, wakifanya zamu kwa kuigiza majukumu tofauti. Baada ya kila onyesho, waulize washiriki ni kwa jinsi gani wanaweza kuwa kama Msamaria mwema.

  • Andika mifano michache ya hali ambazo mtu fulani angehitaji msaada, na ficha karatasi chumbani. Waombe watoto watafute karatasi na kueleza jinsi gani wanaweza kuonyesha ukarimu kwa mtu katika hali hiyo.

  • Imba pamoja na watoto “Yesu Alisema Mpende Kila Mtu” na “Ukarimu Unaanza na Mimi.” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 61, 145. Wagawanye watoto katika jozi, na alika kila jozi kufikiria njia kadhaa ambazo wanaweza kuonyesha upendo au wema kwa wengine. Omba kila jozi kushiriki mawazo yao pamoja na darasa.

  • Waalike watoto kuandika njia ambazo wanaweza kuonyesha upendo kwa wengine kwenye vipande vidogo vya karatasi. Fanya mnyororo wa karatasi kutoka kwenye vipande hivi na kuwaalika watoto kutundika mnyororo wa karatasi nyumbani kwao, ambapo unaweza kuwakumbusha kuwa wakarimu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

Mathayo 18:21–35

Baba wa Mbinguni atanisamehe ninapowasamehe wengine.

Watoto wanapokua, kusamehe kunaweza kuwa vigumu. Fumbo la mtumishi asiye na huruma linaweza kuwa njia ya kukumbukwa kuwafundisha kwamba Baba wa Mbinguni anatutaka tumsamehe kila mmoja.

Shughuli za Yakini

  • Soma Mathayo 18:23–35 pamoja na watoto; eleza kwamba bwana au mfalme inawakilisha Baba wa Mbinguni, watumishi wanatuwakilisha sisi, na mtumishi mwenzetu anawakilisha wale wanaotukosea. Waulize watoto, “Ni lini uliona vigumu kumsamehe mtu fulani? Uliachaje hali hiyo ya hisia zenye uchungu? Ni wakati gani ulipohitaji kusamehewa kwa kufanya uchaguzi mbaya?

  • Onyesha video ya “Samehe Kila Mtu katika Makosa Yao: Fumbo la mtumishi asiye na huruma” (LDS.org) kuwasaidia watoto kuvuta taswira ya fumbo hili.

  • Andika katika ubao hesabu ya kuzidisha 70 × 7 na wasaidie watoto kuitatua. Muombe mmoja asome Mathayo 18:21–22, na eleza kwamba Yesu alitumia namba hii kutufundisha kwamba tunapaswa kusahau.

  • Mpatie kila mtu kipande cha karatasi, na waalike watoto kuchora picha ya mtoto akiwa si mkarimu kwa mtoto mwingine. Kisha waulize kubadilishana karatasi zao na jirani zao na kuchora upande wa nyuma wa karatasi jipya jinsi wanaweza kuonyesha msamaha kwa wengine.

  • Waombe watoto kukusaidia ufikirie hali chache ambapo mtu fulani atapaswa kusamehe mtu mwingine. Waalike watoto kuigiza jinsi wangeweza kuonyesha msamaha katika hali hizo.

  • Imba pamoja na watoto “Nisaidie, Baba yangu.” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99. Wasaidie watoto kuelewa kila mstari wa wimbo na kile unatufundisha kuhusu kusamehe wengine.

Luka 10:30–37

Ninaweza kuwapenda na kuwatumikia wengine, hususani wale wenye uhitaji.

Tafakari nyakati katika maisha yako ambapo mtu fulani alikuwa “Msamaria mwema” kwako. Unawezaje kuwahamasisha watoto kuwa “wasamaria wema” kwa wengine?

Shughuli za Yakini

  • Mpatie kila mtoto sehemu ya fumbo la Msamaria mwema ili achore. Waalike kuweka picha zao kwa mpangilio na zitumie kusimulia hadithi.

  • Eleza kwa watoto kwamba Wayahudi hakuwapenda Wasamaria kabisa kiasi kwamba walisafiri kutoka Yerusalemu hadi Galilaya, walikuwa wakipita kuzunguka Samaria kuepuka kuingiliana na Wasamaria (ona Ramani za Biblia, na. 1. “Ramani ya Eneo Takatifu”). Kwa nini Yesu Alimtumia Msamaria kama mfano wa ukarimu katika fumbo? Hii hadithi inatufundisha nini kuhusu kuwasaidia wengine wenye uhitaji? (Ona pia Mosia 4:16–22.)

  • Waombe watoto kushiriki uzoefu ambapo mtu fulani alikuwa kama Msamaria mwema kwao.

  • Wape changamoto watoto kuweka lengo la kuwa kama Msamaria mwema wiki hii. Kwa mfano, je, wanamfahamu mtu fulani ambaye ni mgonjwa au mpweke? Au mtu fulani ambaye haji kanisani kila mara? Waulize watoto ni jinsi gani wanaweza kumsaidia mtu huyo.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki pamoja na familia lengo lao la kuwa kama Msamaria mwema wiki hii.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wafundishe watoto kuandika Misukumo. Kama watoto watajifunza tabia ya kuandika misukumo, itawasaidia kugundua na kumfuata Roho. Watoto wanaweza kuandika misukumo kwa kuweka alama maandiko, kuchora picha, au kuweka kumbukumbu rahisi katika jarida.

Picha
ukurasa wa shughuli: Ninaonyesha upendo wangu

Chapisha