Njoo, Unifuate
Mei 13–19. Mathayo 19–20; Marko 10; Luka 18: ‘Nimepungukiwa na Nini Tena?’


“Mei 13–19. Mathayo 19–20; Marko10; Luka 18: ‘Nimepungukiwa na Nini Tena?’“ Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Mei 13–19. Mathayo 19–20; Marko 10; Luka 18,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Wafanyakazi katika shamba la mzabibu

Mei 13–19.

Mathayo 19–20; Marko 10; Luka 18

“Nimepungukiwa na Nini Tena?”

Soma Mathayo 19–20; Marko 10; na Luka 18, ukiwa na watoto unaowafundisha akilini Andika minong’ono yoyote unayoipata. Maandalizi yako yatakusaidia kufundisha watoto kile wanachohitajika kujua kutoka kwenye sura hizi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Alika watoto kuelezea darasa kitu wanachokipenda kuhusu familia yao. Unaweza pia kuwaomba wazazi wa watoto kutoa picha za familia zao kwa ajili ya watoto wao kushiriki na darasa.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

Marko 10:6–8

Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kuoana katika hekalu na kuwa na familia za milele.

Ni kwa jinsi gani watoto unaowafundisha wananufaika kutokana na kujifunza kuhusu fundisho la ndoa ya milele? Inaweza msaada kurejea kwenye “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu” (Ensign au Liahona, Nov. 2010, 129)

Shughuli za Yakini

  • Wasomee Marko 10:6–8 watoto, na uonyeshe picha ya wanandoa. Waombe watoto kuota mwanaume na mwanamke wakati wanasikia ukisoma maneno mwanaume na mwanamke. Elezea kuwa Baba wa Mbinguni anakusudia mwanaume na mwanamke kuoana (ona Mwanzo 1:27–28).

  • Onyesha picha za familia na hekalu. Elezea kwamba Baba wa Mbinguni anatutaka tufunganishwe na familia zetu katika hekalu ili tuweze kuwa nao milele. Kuwa na usikivu kwa watoto wale ambao wazazi wao bado hawajafunganishwa.

  • Imba “Familia Yenye Furaha,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 198 Waalike watoto kujiota wenyewe kila wanapoimba “Mimi,” “mimi,” “sisi,” “sisi.” Shughuli hii inaweza kurudiwa mara kadhaa. Waalike watoto kushiriki vitu vya burudani walivyofanya na familia zao. Kwa nini wanashukuru kwa ajili ya familia zao?

  • Imba wimbo kuhusu hekalu au familia, kama vile “Ninapenda Kuona Hekalu” au “Famlilia Zinaweza Kuwa Pamoja Milele,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 95, 188. Waache watoto washike picha za mahekalu au familia, na waalike wazishikilie picha zao juu wakati wanaimba “hekalu” au “familia.” Kwa nini ni muhimu kufunga ndoa katika hekalu?

Picha
wanandoa wakubwa mbele ya hekalu

Ndoa ya Milele ni sehemu ya mpango wa Mungu.

Marko 10:13–16

Yesu anawataka watoto wadogo waje Kwake ili awabariki.

Simulizi hii inatoa nafasi ya kuwasaidia watoto kuhisi kiasi gani Yesu anawapenda.

Shughuli za Yakini

  • Kwa maneno yako mwenyewe, shiriki simulizi kutoka Marko 10:13–16. Unaweza pia kuonyesha video “Waache Watoto Wadogo Waje Kwangu” (LDS.org). Wakati gani watoto wamehisi upendo wa Yesu kwao? Toa ushuhuda wako kwa watoto kwamba Yesu anawapenda na anataka kuwabariki.

  • Onyesha picha Kristo na Watoto (Kitabu cha Sanaa ya Injili, namba. 47). Elezea kwamba kama tunataka kuwa kama watoto waliokaa pembeni kwa Yesu basi tufuate amri Zake na kumpenda Yeye na watu wengine. Ni nini watoto wanaweza kufanya kuwa kama watoto waliokaa pembeni kwa Yesu?

  • Acha watoto wachore picha za wao wenyewe wakibarikiwa na Yesu (ona Marko 10:16).

Marko 10:17–22

Kama tunatii amri, tunaweza kupokea uzima wa milele.

Yesu alimfundisha kijana tajiri kwamba kupata uzima wa milele—Maisha kama aliyonayo Baba wa Mbinguni—alitakiwa kutiii amri.

Shughuli za Yakini

  • Soma hadithi ya kijana tajiri katika Marko 10:17–22 pamoja na watoto. (Ona pia “Sura 42: Kijana Tajiri,” Hadithi za Agano Jipya, 105–6, au video zinazoambatana katika LDS.org.) Waombe kusikiliza kile Yesu alimwambia kijana kufanya na jinsi kijana alijibu.

  • Simulia moja au hadithi zaidi kuhusu watoto ambao wanaomba ushauri au maelekezo kutoka kwa wazazi wao lakini hawafuati au kutii. Ni baadhi ya vitu gani Baba wa Mbinguni anatuambia tufanye? Tunajisikiaje tunapotii amri Zake?

  • Shiriki uzoefu wako wakati ulipokea minong’ono binafsi kufanya kitu kuwa bora.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

Marko 10:6–8

Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kuoana katika hekalu na kuwa na familia za milele.

Vitu ambavyo Yesu alifundisha kuhusu ndoa vinaweza kuwasaidia watoto wakati wanakabiliwa na jumbe zilizo kinyume katika ulimwengu.

Shughuli za Yakini

  • Muombe mtoto mmoja asome Marko 10:6–8 kwa sauti. Eleza kwamba ambatana inamaana ku “baki kwenye” au “shikilia kwa karibu kwenye” kitu. Kwa nini ni muhimu kwamba waume na wake waungane pamoja, kupendana, na kufanya kazi kwa ubia?

  • Shiriki kauli ifuatayo kutoka “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu.” na wasaidie watoto kuelewa inamaanisha nini: “Jinsia ni sifa muhimu ya mtu kabla ya kuzaliwa duniani, hapa duniani, na utambulisho wa milele na dhumuni.”

  • Waombe watoto wakusaidie kufikiria majibu ya swali kama “Kwa nini familia ni muhimu katika Kanisa?” au “Kwa nini ni muhimu kwako kufunga ndoa katika hekalu?” Imba kwa pamoja “Familia Zinaweza Kuwa Pamoja Milele.” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 188. Shiriki ushuhuda wako wa ndoa ya milele na familia pamoja na watoto. Waalike kushiriki ushuhuda wao pia.

  • Mwalike kila mtoto kusoma andiko kutoka katika orodha hii: Marko 10:6–8; 1 Wakorintho 11:11; M&M 42:22; 131:1–4; na Musa 3:18, 21–24. Maandiko haya yanafundisha nini kuhusu ndoa?

Marko 10:17–22

Yesu Anaweza kunisaidia kujua kile ninahitaji kufanya ili kuendelea.

Kijana tajiri alimtafuta Yesu na kupokea maagizo ambayo yalikuwa hususani kwa ajili yake. Unawezaje kuwahamasisha watoto kutafuta mwongozo kama huo katika maisha yao wenyewe?

Shughuli za Yakini

  • Waombe watoto kutafuta mstari katika Marko 10:17–22 unaoelezea picha katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Nifuate—Kwa Watu Binafsi na Familia. Eleza kwamba ushauri wa Yesu Alioutoa kwa kijana ulikuwa binafsi, na sote tunaweza kupokea mwongozo binafsi kutoka kwa Bwana kupitia Roho.

  • Someni pamoja Marko 10:17–22. Waalike watoto kandika katika ubao amri ambazo Mwokozi alimwambia kijana tajiri kuzitii (ona mstari 19). Ni nini kingine alitakiwa kufanya? (Ona mstari 21). Wahimize watoto kufikiria kuhusu vitu wanavyoweza kuhitaji kuanza kuvifanya au kuacha kufanya ili kumfuata Yesu vizuri. Ni zipi baadhi ya njia tunazoweza kujua kile Yesu anatutaka tufanye.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kuwaambia familia zao kwa nini wanawashukuru, pengine kwa kuandika ujumbe na kuwapatia wazazi wao au kwa kushiriki shuhuda zao juu ya familia wakati wa jioni ya familia nyumbani.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kuwa na usikivu kwa watoto. Ni kwa jinsi gani watoto katika darasa lako wanajibu shughuli za kujifunza? Kama hawaonyeshi kushiriki, inaweza kuwa wakati mwafaka wa kujaribu shughuli nyingine au kufanya matembezi mafupi, ya utulivu. Kwa upande mwengine, kama unagundua kwamba watoto wanashiriki na kujifunza kutoka kwenye sehemu fulani ya somo, usijisikie kushinikizwa kuendelea mbele ili kuhakikisha unapitia nyenzo zote za somo.

Chapisha