Sura ya 42
Mvulana Tajiri
Siku moja mvulana tajiri alimjia Yesu na kumuuliza kile anachopaswa kufanya ili apate kwenda mbinguni.
Mwokozi alimwambia awapende na kuwaheshimu baba na mama yake na asiue mtu yeyote au kudanganya au kuiba. Mvulana tajiri alisema alikuwa daima akitii amri.
Yesu alimwambia mvulana yule kwamba alihitaji kufanya kitu kingine kimoja. Alihitaji kuuza kila kitu alichokuwanacho na kutoa pesa hizo kwa masikini. Kisha mvulana huyo alipaswa kumfuata Yeye.
Mvulana tajiri hakutaka kutoa vyote alivyokuwanavyo. Alipenda vile vitu alivyokuwanavyo zaidi ya vile alivyompenda Mungu. Mvulana aliondoka akihuzunika.
Mwokozi aliwaambia wanafunzi Wake kwamba ni vigumu kwa wale wapendao mali kwenda mbinguni. Wanafunzi hawakuelewa. Waliuliza nani anaweza kuishi na Mungu. Yesu alisema kwamba watu wanaomtumainia Mungu na kumpenda zaidi ya kitu chochote kingine wanaweza kuishi Naye mbinguni.
Marko 10:23–30 (ona rejeo chini ya ukurasa 27a)