Scripture Stories
Sura ya 57: Watu Waovu Wanamwua Stefano


Sura ya 57

Watu Waovu Wanamwua Stefano

Picha
Mitume wakimsaidia mtu

Viongozi wengi wa Kiyahudi walifikiri kwamba miujiza ingekoma Yesu alipokufa. Lakini, Mitume pia walifanya miujiza. Watu wengi waliamini katika Yesu Kristo na kujiunga na Kanisa.

Picha
askari wakimtisha mtu

Hii iliwakasirisha viongozi wengi wa Kiyahudi. Waliwaweka Petro na Yohana gerezani. Mfalme Herode Agripa alifanya Mtume Yakobo auwawe.

Picha
Mtume Stefano

Mitume waliwaita watu saba wasaidie kuongoza Kanisa. Mmoja alikuwa mtu mwadilifu aliyeitwa Stefano. Alifundisha injili kwa watu wengi. Baadhi ya watu walidanganya na kusema kwamba Stefano alizungumza kinyume cha sheria ya Wayahudi. Walimpeleka kuhukumiwa na viongozi wa Wayahudi.

Picha
Stefano akiwafundisha watu

Stefano aliwaambia viongozi kwamba walikuwa waovu. Alisema kwamba walikuwa wamemwua Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

Picha
Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wakimtokea Stefano

Kisha Stefano alitazama juu mbinguni na kuwaona Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Alipowaambia viongozi kile alichoona, walikasirika sana.

Picha
watu wakimpiga mawe Stefano

Walimchukua Stefano nje ya mji ili kumwua kwa kumpiga na mawe. Waliweka nguo zao miguuni mwa kijana mmoja aliyeitwa Sauli. Stefano alipokuwa anakufa, alimwomba Mungu aichukue roho yake mbinguni. Pia alimwomba Mungu awasamehe wale ambao walikuwa wakimwua. Kisha alikufa.

Chapisha