Sura ya 52
Mashitaka ya Yesu
Viongozi wa Wayahudi walituma watu wenye mapanga na fimbo kwenye Bustani ya Gethsemane.
Yuda Iskariote alikuwa pamoja nao. Makuhani wakuu walikuwa wamemlipa Yuda ili kuwaonyesha watu wale mahali Yesu alipokuwa.
Yuda aliwaonyesha watu wale Yesu alikuwa yupi kwa kumbusu. Watu wale walimchukua Yesu. Walimkejeli na kumpiga. Kisha walimpeleka Yesu kwa kuhani mkuu, Kayafa.
Viongozi wa Kiyahudi walimwuliza Yesu maswali. Walisema kwamba alikuwa amevunja sheria kwa kusema kwamba Yeye alikuwa Mwana wa Mungu. Yesu aliwaambia kwamba Yeye alikuwa Mwana wa Mungu. Walisema Yesu alikuwa na hatia na alipaswa afe.
Viongozi wa Kiyahudi hawakuwa na mamlaka ya kumwua Yesu. Walimpeleka kwa Pontio Pilato, ambaye angeweza kumhukumu Yesu kifo. Viongozi wa Kiyahudi walimwambia Pilato kwamba Yesu alikuwa amewafundisha watu kutotii sheria ya Kirumi.
Pilato hakufikiri Yesu alikuwa amefanya chochote kibaya. Pilato alitaka kumwachia Yesu. Umati ulitaka Yesu asulubiwe.
Pilato bado alitaka kumwachia Yesu. Lakini makuhani na watu waliendelea kupiga kelele kwamba walitaka Yesu asulubiwe.
Pilato aliosha mikono yake. Alisema kwamba hakuhusika na kifo cha Yesu. Watu walisema kwamba wangewajibika kwa ajili ya kifo Chake. Pilato aliwaambia askari wake wamsulubishe Yesu.