Sura ya 46
Ujio wa Pili
Yesu alikuwa kwenye Mlima wa Mizeituni. Wanafunzi Wake walitaka kumuuliza Yesu maswali kadhaa. Waliuliza ni lini waovu wangeangamizwa. Walitaka pia kujua lini Yesu angekuja tena.
Yesu aliwaambia kwamba kabla ya Ujio Wake wa Pili, manabii wa uwongo wangedai kuwa wao ndio Kristo. Watu wengi wangewafuata. Lakini kama wafuasi Wake wangetii maneno Yake, wasingepumbazwa na manabii wa uongo. Wangeokolewa.
Yesu pia alisema kwamba kabla hajaja tena, kutakuwa na vita vingi, njaa, magonjwa mabaya, na matetemeko ya ardhi. Watu wengi wataacha kuwasaidia wengine na kuwa waovu.
Injili itahubiriwa duniani kote, lakini watu wengi hawatasikiliza.
Jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka kutoka mbinguni.
Yesu Kristo atakapokuja tena, watu watamuona akija kutoka mawinguni kwa nguvu na utukufu mkuu. Atawatuma malaika Wake wawakusanye wenye haki pamoja.
Tunaweza kujiandaa kwa ajili ya Ujio wa Pili kwa kufanya kile kilicho chema. Tutakapoona ishara ambazo Yesu aliahidi, tutajua kwamba ujio wa Mwokozi u karibu. Hakuna anayejua kwa uhakika lini Yesu atakuja tena. Kama tumejiandaa, tunaweza kuwa Naye.