Scripture Stories
Sura ya 5: Yesu Kristo Azaliwa


Sura ya 5

Yesu Kristo Azaliwa

Picha
Rumi ikiwatoza watu kodi

Mfalme mkuu wa Rumi aliweka sheria kwamba kila mtu lazima alipe kodi. Yusufu na Mariamu waliishi Nazareti. Iliwabidi waende maili 65 (105km) hadi Bethlehemu kulipa kodi zao.

Picha
Yusufu na Mariamu wakisafiri

Haikuwa rahisi kwa Mariamu kusafiri hadi Bethlehemu. Mtoto wake punde angezaliwa.

Picha
Yusufu na Mariamu kwenye nyumba ya wageni

Wakati Yusufu na Mariamu walipofika Bethlehemu, vyumba vyote vilikuwa vimejaa watu. Mariamu na Yusufu walilazimika kukaa ndani ya zizi. Zizi ni mahali ambapo wanyama huwekwa.

Picha
Yusufu, Mariamu, na mtoto Yesu

Hapo mtoto alizaliwa. Mariamu alimfunika kwa nguo na kumlaza katika hori. Yusufu na Mariamu walimwita mtoto Yesu.

Picha
malaika akiwatokea wachungaji

Usiku ambao Yesu alizaliwa, wachungaji walikuwa wakichunga kondoo wao makondeni karibu na Bethlehemu. Malaika aliwatokea. Wachungaji waliogopa.

Picha
malaika akiwatokea wachungaji

Malaika aliwaambia wasiogope. Alikuwa na habari njema: Mwokozi, Yesu Kristo, alikuwa amezaliwa Bethlehemu. Wangemkuta amelala katika hori.

Picha
Wachungaji wakimtembelea mtoto Yesu

Wachungaji walienda Bethlehemu, ambako walimuona mtoto Yesu.

Picha
Wachungaji wakizungumza na watu

Wachungaji walifurahi kumwona Mwokozi. Waliwaambia watu wengine kuhusu yote waliyokuwa wamesikia na kuona.

Chapisha