Sura ya 4
Yusufu na Malaika
Picha
Yusufu na Mariamu
Yusufu alikuwa mtu mwema na mkarimu. Yeye na Mariamu walikuwa waoane. Alipofahamu kwamba Mariamu alikuwa mja mzito, hakujua nini cha kufanya. Kwa sababu mtoto hakuwa wake, alifikiria alipaswa kutomuoa.
Picha
malaika akimtokea Yusufu
Usiku mmoja malaika alimjia Yusufu katika ndoto na kumwambia kwamba mtoto wa Mariamu alikuwa Mwana wa Mungu. Malaika alimwambia Yusufu amwoe Mariamu na amwite mtoto wake Yesu. Yesu alikuwa awe Mwokozi wa ulimwengu.
Picha
Yusufu na Mariamu wakioana.
Yusufu alimtii malaika na kumwoa Mariamu.