Sura ya 31
Yesu Anamponya Kiziwi
Picha
watu wakimleta mtu kwa Yesu
Watu fulani walimleta mtu kwa Yesu. Mtu huyo alikuwa kiziwi na hakuweza kuzungumza vizuri. Watu walimtaka Mwokozi amponye.
Picha
Yesu akimponya mtu
Yesu alimwongoza mtu huyo mbali na wengine. Aliweka vidole vyake katika masikio ya mtu huyo. Aligusa ulimi wa mtu huyo na kumbariki.
Picha
mtu akitabasamu
Sasa mtu huyo angeweza kusikia na kuzungumza. Watu wangeweza kumwelewa. Yesu aliwasihi watu wasimwambie yeyote kile kilichotokea, lakini watu walimwambia kila mtu.