Scripture Stories
Sura ya 31: Yesu Anamponya Kiziwi


Sura ya 31

Yesu Anamponya Kiziwi

Picha
watu wakimleta mtu kwa Yesu

Watu fulani walimleta mtu kwa Yesu. Mtu huyo alikuwa kiziwi na hakuweza kuzungumza vizuri. Watu walimtaka Mwokozi amponye.

Picha
Yesu akimponya mtu

Yesu alimwongoza mtu huyo mbali na wengine. Aliweka vidole vyake katika masikio ya mtu huyo. Aligusa ulimi wa mtu huyo na kumbariki.

Picha
mtu akitabasamu

Sasa mtu huyo angeweza kusikia na kuzungumza. Watu wangeweza kumwelewa. Yesu aliwasihi watu wasimwambie yeyote kile kilichotokea, lakini watu walimwambia kila mtu.

Chapisha