Scripture Stories
Sura ya 30: Mkate wa Uzima


Sura ya 30

Mkate wa Uzima

Picha
watu katika mashua

Siku iliyofuata watu wengi walijaribu kumtafuta Yesu. Walimfuata Kapernaumu kwa mashua.

Picha
Yesu kando ya bahari

Yesu alijua kwamba walitaka awalishe tena.

Picha
Yesu akiwafundisha watu

Yesu aliwafundisha kwamba mkate ungeweza kuwaweka hai kwa muda mfupi tu. Alisema kwamba kulikuwa na aina nyingine ya mkate ambao walipaswa kuutafuta —Mkate wa Uzima. Aliwaambia kwamba Yeye alikuwa Mkate wa Uzima.

Picha
Yesu akiwafundisha watu

Yesu aliwafundisha watu kwamba angetoa maisha Yake kama dhabihu kwa ajili yao. Alisema kwamba kama wangemfuata na kumwamini Yeye, wangepata uzima wa milele.

Chapisha