Sura ya 30
Mkate wa Uzima
Picha
watu katika mashua
Siku iliyofuata watu wengi walijaribu kumtafuta Yesu. Walimfuata Kapernaumu kwa mashua.
Picha
Yesu kando ya bahari
Yesu alijua kwamba walitaka awalishe tena.
Picha
Yesu akiwafundisha watu
Yesu aliwafundisha kwamba mkate ungeweza kuwaweka hai kwa muda mfupi tu. Alisema kwamba kulikuwa na aina nyingine ya mkate ambao walipaswa kuutafuta —Mkate wa Uzima. Aliwaambia kwamba Yeye alikuwa Mkate wa Uzima.
Picha
Yesu akiwafundisha watu
Yesu aliwafundisha watu kwamba angetoa maisha Yake kama dhabihu kwa ajili yao. Alisema kwamba kama wangemfuata na kumwamini Yeye, wangepata uzima wa milele.