Sura ya 37
Wenye Ukoma Kumi
Yesu alienda kwenye mji mdogo ambapo aliwaona wenye ukoma kumi. Wenye ukoma ni watu ambao ni wagonjwa. Ugonjwa wao huwasababishia kupata vidonda vibaya kote katika miili yao.
Madaktari hawakuweza kuwasaidia wenye ukoma. Watu walikuwa na hofu kuwakaribia. Hawakutaka kuwa wagonjwa pia.
Wenye ukoma walimsihi Yesu awaponye. Walijua angeweza kufanya vidonda vyao vipotee.
Yesu aliwataka wawe wazima. Aliwaambia waende wajionyeshe kwa makuhani.
Walipokuwa njiani kwenda kwa makuhani, wenye ukoma kumi waliponywa. Vidonda vyao vilikuwa vimetoweka.
Mmoja wa wenye ukoma alijua kwamba Yesu alikuwa amewaponya. Alirudi kumshukuru Yesu. Yesu aliuliza walipokuwa wenye ukoma wengine tisa. Hawakuwa wamerudi. Yesu alimwambia mwenye ukoma aliyekuwa amemshukuru kwamba imani ya mwenye ukoma huyo ilikuwa imemponya.