Scripture Stories
Sura ya 37: Wenye Ukoma Kumi


Sura ya 37

Wenye Ukoma Kumi

Picha
Yesu akiwakaribia wenye ukoma

Yesu alienda kwenye mji mdogo ambapo aliwaona wenye ukoma kumi. Wenye ukoma ni watu ambao ni wagonjwa. Ugonjwa wao huwasababishia kupata vidonda vibaya kote katika miili yao.

Picha
watu wakikimbia kutoka kwa mwenye ukoma

Madaktari hawakuweza kuwasaidia wenye ukoma. Watu walikuwa na hofu kuwakaribia. Hawakutaka kuwa wagonjwa pia.

Picha
wenye ukoma wakizungumza na Yesu

Wenye ukoma walimsihi Yesu awaponye. Walijua angeweza kufanya vidonda vyao vipotee.

Picha
wenye ukoma wakiondoka

Yesu aliwataka wawe wazima. Aliwaambia waende wajionyeshe kwa makuhani.

Picha
wenye ukoma wakitazama mikono yao

Walipokuwa njiani kwenda kwa makuhani, wenye ukoma kumi waliponywa. Vidonda vyao vilikuwa vimetoweka.

Picha
mwenye ukoma mmoja akimshukuru Yesu

Mmoja wa wenye ukoma alijua kwamba Yesu alikuwa amewaponya. Alirudi kumshukuru Yesu. Yesu aliuliza walipokuwa wenye ukoma wengine tisa. Hawakuwa wamerudi. Yesu alimwambia mwenye ukoma aliyekuwa amemshukuru kwamba imani ya mwenye ukoma huyo ilikuwa imemponya.

Chapisha