Sura ya 48
Talanta
Yesu aliwaambia wanafunzi Wake hadithi ya mtu aliyewapa watumishi wake talanta kadhaa. Talanta ilikuwa ni kiasi kikubwa cha pesa.
Mtu yule alimpa mtumishi mmoja talanta tano. Alimpa mtumishi mwingine talanta mbili. Alimpa mtumishi wa tatu talanta moja. Kisha mtu yule akaenda safari.
Mtumishi aliyekuwa na talanta tano alifanya kazi kwa bidii. Alipata talanta tano zaidi. Sasa alikuwa na talanta kumi.
Mtumishi aliyekuwa na talanta mbili pia alifanya kazi kwa bidii. Alipata talanta mbili zaidi. Sasa alikuwa na talanta nne.
Mtumishi aliyekuwa na talanta moja aliifukia ardhini. Alikuwa na hofu angeipoteza. Hakufanya kazi kupata talanta yoyote zaidi.
Mtu yule aliporudi, aliwauliza watumishi kile walichokuwa wamefanya na talanta zake.
Mtumishi wa kwanza alimletea talanta kumi. Mtu yule alikuwa na furaha. Alimfanya mtumishi kuwa kiongozi juu ya mambo mengi na kumwambia awe na furaha.
Mtumishi wa pili alimletea mtu yule talanta nne. Hii pia ilimfanya mtu yule awe na furaha. Alimfanya mtumishi wa pili kuwa kiongozi juu ya mambo mengi na akamwambia awe na furaha.
Mtumishi wa tatu alimrudishia mtu yule talanta ile aliyokuwa ameifukia. Mtu yule hakuwa na furaha. Alisema yule mtumishi alikuwa mvivu. Alipaswa kufanya kazi kwa bidii ili apate talanta zaidi.
Mtu yule aliichukua talanta kutoka kwa mtumishi wa tatu na kumpa mtumishi wa kwanza. Kisha akamfukuzia mbali mtumishi mvivu. Mtu yule katika hadithi ni kama Yesu. Sisi ni kama wale watumishi. Yesu atahukumu jinsi kila mmoja wetu anavyotumia karama ambazo tumepewa.