Scripture Stories
Sura ya 20: Yesu Anafundisha kuhusu Sala


Sura ya 20

Yesu Anafundisha kuhusu Sala

Picha
Yesu akiwafundisha wanafunzi

Yesu aliwafundisha wanafunzi Wake jinsi ya kusali. Alisema kwamba baadhi ya watu husali ili tu waonekane na wengine kwamba wanasali. Yesu alifundisha kwamba tunapaswa kutoa sala zetu binafsi mahali ambapo tunaweza kuwa peke yetu, kama inawezekana.

Picha
Yesu akiwafundisha wanafunzi

Alisema kwamba baadhi ya watu husema maneno yale yale tena na tena wanaposali. Hawafikirii hasa kuhusu kile wanachosema. Yesu alisema kwamba tunapaswa kusali kwa dhati kwa kile tunachohitaji.

Picha
Yesu akisali na wanafunzi

Mwokozi alisali ili kuwaonyesha wanafunzi Wake jinsi ya kusali. Alianza kwa kusema, “Baba yetu … uliye mbinguni.” Alimtukuza Baba wa Mbinguni na kisha akamwomba usaidizi. Alisema “amina” mwishoni mwa sala Yake. Baadaye, Yesu aliwaambia wanafunzi Wake kusali kwa Baba katika jina Lake. Aliahidi kwamba Baba wa Mbinguni angejibu sala zao.

Chapisha