Sura ya 21
Yesu Anaamuru Upepo na Mawimbi
Picha
mashua kwenye bahari yenye tufani
Yesu na wanafunzi Wake walikuwa katika mashua kwenye Bahari ya Galilaya. Yesu alilala. Upepo ulianza kuvuma kwa nguvu, na mawimbi yalikuwa yakijaza mashua kwa maji. Wanafunzi walikuwa na hofu kwamba ingezama. Walimwamsha Yesu na kumsihi asaidie.
Picha
Yesu akiamuru tufani
Mwokozi aliamuru upepo ukome kuvuma na mawimbi yatulie. Upepo ulikoma, na bahari ikatulia.
Picha
Yesu akiwafundisha wanafunzi
Yesu aliwauliza wanafunzi ni kwa nini walikuwa na hofu. Alisema kwamba walipaswa kuwa na imani zaidi. Walishangaa ni mtu wa aina gani anayeweza kuamuru hata upepo na bahari.