Sura ya 54
Yesu Amefufuka
Mwili wa Mwokozi ulikuwa kaburini hadi Jumapili asubuhi. Kisha malaika wawili walikuja na kulivingirisha jiwe kutoka kwenye kaburi.
Mathayo 28:1–2 (ona rejeo chini ya ukurasa 2a); Luka 24:1–4
Mwanamke ambaye Yesu alikuwa amemponya aliyeitwa Mariamu Magdalene alienda kaburini. Alistaajabu kuona kwamba jiwe lilikuwa limeondolewa. Mwili wa Yesu haukuwa kaburini.
Alikimbia kuwaambia Petro na Yohana kwamba mtu alikuwa ameuchukua mwili wa Mwokozi. Hakujua pale ulipokuwa.
Petro na Yohana walikimbia kwenda kaburini. Walikuta kitambaa ambacho Yesu alikuwa amezikwanacho, lakini mwili wa Yesu haukuwepo. Petro na Yohana hawakujua nini cha kufanya. Walienda nyumbani.
Mariamu Magdalene alibaki kaburini, akilia. Alipotazama ndani ya kaburi tena, aliwaona malaika wawili.
Walimwuuliza Mariamu Magdalene kwa nini alikuwa akilia. Alisema mtu alikuwa ameuchukua mwili wa Yesu. Hakujua pale ulipokuwa.
Aligeuka na kumwona mtu. Alidhani alikuwa mtunza bustani. Alimuliza kwa nini alikuwa akilia. Alimuuliza Yeye kama alikuwa anajua pale mwili wa Yesu ulipokuwa.
Kisha mtu yule akasema, “Mariamu,” na alijua alikuwa ni Yesu. Alimsihi awaeleze Mitume kwamba Yeye alikuwa amefufuka.
Mariamu Magdalene na wanawake wengine waliwaambia Mitume kwamba Yesu alikuwa amefufuka. Mara ya kwanza Mitume hawakuwaamini.
Baadaye, wakati Mitume walipokuwa wakizungumza kati yao, Yesu alikuja chumbani. Mitume waliogopa. Bado walidhani Yeye amekufa.
Mwokozi aliwaambia waguse mikono na miguu Yake. Alikuwa amefufuka—mwili na roho Yake vilikuwa vimeungana tena.
Mitume walikuwa na furaha kumwona Yeye. Aliwaomba wampe chakula. Walimpa samaki na sega la asali. Alikula.
Yesu Kristo alikuwa ndiye mtu wa kwanza kufufuka. Wengi wengine walifufuliwa na kuonekana na watu walioishi Yerusalemu. Yesu alikuwa amesema, “Mimi ndiye ufufuo, na uzima.” Kwa sababu alishinda kifo, sote tutafufuliwa siku moja.