Scripture Stories
Sura ya 54: Yesu Amefufuka


Sura ya 54

Yesu Amefufuka

Picha
malaika wakivingirisha jiwe kutoka kwenye kaburi

Mwili wa Mwokozi ulikuwa kaburini hadi Jumapili asubuhi. Kisha malaika wawili walikuja na kulivingirisha jiwe kutoka kwenye kaburi.

Mathayo 28:1–2 (ona rejeo chini ya ukurasa 2a); Luka 24:1–4

Picha
Mariamu Magdalene

Mwanamke ambaye Yesu alikuwa amemponya aliyeitwa Mariamu Magdalene alienda kaburini. Alistaajabu kuona kwamba jiwe lilikuwa limeondolewa. Mwili wa Yesu haukuwa kaburini.

Picha
Mariamu Magdalene akizungumza na Mitume

Alikimbia kuwaambia Petro na Yohana kwamba mtu alikuwa ameuchukua mwili wa Mwokozi. Hakujua pale ulipokuwa.

Picha
Petro na Yohana kwenye mlango wa kaburi

Petro na Yohana walikimbia kwenda kaburini. Walikuta kitambaa ambacho Yesu alikuwa amezikwanacho, lakini mwili wa Yesu haukuwepo. Petro na Yohana hawakujua nini cha kufanya. Walienda nyumbani.

Picha
malaika wamekaa kaburini

Mariamu Magdalene alibaki kaburini, akilia. Alipotazama ndani ya kaburi tena, aliwaona malaika wawili.

Picha
Mariamu Magdalene akilia

Walimwuuliza Mariamu Magdalene kwa nini alikuwa akilia. Alisema mtu alikuwa ameuchukua mwili wa Yesu. Hakujua pale ulipokuwa.

Picha
Yesu akimyooshea mkono Mariamu Magdalene

Aligeuka na kumwona mtu. Alidhani alikuwa mtunza bustani. Alimuliza kwa nini alikuwa akilia. Alimuuliza Yeye kama alikuwa anajua pale mwili wa Yesu ulipokuwa.

Picha
Mariamu Magdalene amepiga magoti mbele ya Yesu

Kisha mtu yule akasema, “Mariamu,” na alijua alikuwa ni Yesu. Alimsihi awaeleze Mitume kwamba Yeye alikuwa amefufuka.

Picha
Mariamu Magdalene akizungumza na Mitume

Mariamu Magdalene na wanawake wengine waliwaambia Mitume kwamba Yesu alikuwa amefufuka. Mara ya kwanza Mitume hawakuwaamini.

Picha
Yesu akiwatokea Mitume

Baadaye, wakati Mitume walipokuwa wakizungumza kati yao, Yesu alikuja chumbani. Mitume waliogopa. Bado walidhani Yeye amekufa.

Picha
Yesu akiwaonyesha Mitume mikono yake

Mwokozi aliwaambia waguse mikono na miguu Yake. Alikuwa amefufuka—mwili na roho Yake vilikuwa vimeungana tena.

Picha
Mitume wakimpa Yesu chakula

Mitume walikuwa na furaha kumwona Yeye. Aliwaomba wampe chakula. Walimpa samaki na sega la asali. Alikula.

Picha
Viumbe waliofufuka wakiwatokea watu

Yesu Kristo alikuwa ndiye mtu wa kwanza kufufuka. Wengi wengine walifufuliwa na kuonekana na watu walioishi Yerusalemu. Yesu alikuwa amesema, “Mimi ndiye ufufuo, na uzima.” Kwa sababu alishinda kifo, sote tutafufuliwa siku moja.

Chapisha