Scripture Stories
Sura ya 39: Yesu Anamponya Kipofu


Sura ya 39

Yesu Anamponya Kipofu

Picha
Yesu na wanafunzi wakimkaribia kipofu

Siku moja Yesu alikuwa akitembea na wanafunzi Wake. Walimwona mtu aliyekuwa amezaliwa kipofu. Wanafunzi waliuliza kama mtu yule alikuwa kipofu kwa sababu alikuwa ametenda dhambi ama kwa sababu wazazi wake walikuwa wametenda dhambi.

Picha
Yesu akizungumza na kipofu

Mwokozi alisema kwamba si wazazi wala mtu yule aliyekuwa ametenda dhambi. Mtu yule alikuwa kipofu ili kwamba Yesu amponye na kuonyesha watu nguvu ya Mungu.

Picha
Yesu akimponya kipofu

Yesu alitengeneza matope kutoka kwenye udongo. Akayaweka kwenye macho ya kipofu. Yesu alimwambia mtu yule aende akaoshe macho yake.

Picha
kipofu akiosha macho yake

Mara tu mtu yule alipoosha matope kutoka kwenye macho yake, aliona!

Picha
watu wakitabasamu

Jirani zake walipomuona, hawakuwa na uhakika yeye ni nani. Aliwaambia kwamba Yesu alikuwa amemponya. Majirani walimpeleka mtu yule kwa Mafarisayo. Mtu yule aliwaambia Mafarisayo kwamba Yesu alikuwa amemponya.

Picha
watu wakimuuliza maswali kipofu

Baadhi ya Mafarisayo walifikiri Yesu lazima awe mtu mwadilifu. Wengine walifikiri Yeye alikuwa mwenye dhambi. Mtu yule aliposema Yesu alikuwa mtu mwadilifu, baadhi ya Mafarisayo walikasirika na kumtoa mtu huyo nje.

Picha
Yesu akizungumza na mtu

Yesu alimpata mtu yule. Alimuuliza kama aliamini katika Mwana wa Mungu. Mtu yule aliuliza Mwana wa Mungu ni nani. Yesu alisema kwamba Yeye alikuwa Mwana wa Mungu, na mtu yule akamwabudu.

Chapisha