Sura ya 9
Mvulana Yesu
Yesu alilelewa katika mji wa Nazareti. Alijifunza mambo mengi na “akaongezeka nguvu, … na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.”
Yesu alipokuwa na miaka 12, Alienda na Yusufu na Mariamu katika kikundi cha watu kwenye sherehe Yerusalemu. Walikuwa huko kwa siku kadhaa.
Wakati Yusufu na Mariamu walipoondoka kwenda nyumbani, walifikiria kwamba Yesu alikuwa akitembea kurudi Nazareti pamoja na rafiki Zake. Lakini Yesu alikuwa amebaki Yerusalemu.
Wakati Yusufu na Mariamu walipomtafuta Yesu, hawakuweza kumpata. Hakuna yeyote katika kikundi chao aliyekuwa Amemwona. Hivyo Yusufu na Mariamu walirudi Yerusalemu. Walimtafuta Yesu kwa siku tatu. Walihuzunika sana.
Hatimaye walimpata Yesu Hekaluni, akizungumza na baadhi ya walimu. Alikuwa akijibu maswali yao. Walimu walishangazwa na mengi ambayo Yesu aliyajua.
Luka 2:46–47 (ona rejeo chini ya ukurasa 46c)
Mariamu alimwambia Yesu kwamba yeye na Yusufu walikuwa na hofu kumhusu Yeye. Yesu alijibu kwamba alikuwa akifanya kazi ya Baba Yake — kazi ya Mungu. Yusufu na Mariamu hawakuelewa.
Yesu alienda nyumbani Nazareti pamoja na Yusufu na Mariamu na kuwatii.
Yesu alijifunza zaidi na zaidi kuhusu kazi ya Baba Yake wa Mbinguni.
Alikuwa mrefu na mwenye nguvu.
Watu walimpenda. Alifanya kile Mungu alimtaka Yeye afanye.
Mungu Alimpenda.