Scripture Stories
Picha za Nchi Takatifu


Picha za Nchi Takatifu

(Namba katika mabano ni namba za sura za hadithi ambazo zilitendeka mahali ama karibu na mahali picha ilipochukuliwa. )

Picha
Bethlehemu

BethlehemuYesu Kristo alizaliwa katika mji huu. (5, 7)

Picha
hekalu

HekaluHuu ni mfano wa hekalu katikaYerusalemu ambapo Yesu alifundisha injili na kuwafukuza nje watu waliokuwa wakiuza wanyama kwa ajili ya dhabihu. (1, 6, 9, 11, 13, 45, 56)

Picha
ngazi za kwenda hekaluni

Ngazi za kwenda HekaluniHizi ni ngazi halisi zilizoelekeza hekaluni.

Picha
Nazareti

NazaretiYesu alilelewa katika mji huu. (2, 4, 9, 17)

Picha
Yerusalemu

YerusalemuYesu na Mitume Wake walitumia muda mwingi kufundisha katika mji huu. Yesu alikufa na kufufuka hapa. (6, 39–40, 44–57, 63)

Picha
Mto Yordani

Mto YordaniYohana Mbatizaji alimbatiza Yesu Kristo mahali fulani katika mto huu. (10)

Picha
Nyika za Yudea

Nyika za YudeaYesu Kristo alifunga na kujaribiwa na ibilisi nyikani baada ya ubatizo Wake. (11)

Picha
Samaria

SamariaYesu alimfundisha mwanamke kuhusu maji ya uzima kisimani katika nchi hii. Wengi wa Wayahudi waliwachukia watu wa Samaria. (15, 58)

Picha
Bahari ya Galilaya

Galilaya na Bahari ya GalilayaWatu wengi wanaamini upande huu wa mlima ndipo mahali Yesu alitoa Mahubiri ya Mlimani. Bahari ya Galilaya iko kwa nyuma. Yesu alifundisha injili kwa watu wengi, ikijumuisha Mitume Wake, karibu na hapa. Yesu alituliza dhoruba kwenye Bahari ya Galilaya. (18–22, 29, 34, 36)

Picha
Kapernaumu

KapernaumuMagofu haya yako katika mji wa Kapernaumu. Yesu alifanya miujiza mingi katika mji huu. (23–25, 30)

Picha
Kaisaria Filipi

Kaisaria FilipiKatika eneo hili Yesu alishuhudia kifo Chake na Ufufuko Wake, na Petro alishuhudia kwamba Yesu ndiye Mwana wa Mungu. (32)

Picha
Yeriko

YerikoKatika fumbo la Msamaria mwema, mtu alikaribia kuuwawa alipokuwa akisafiri njiani kwenda kwenye mji huu. (35)

Picha
Mlima Tabori

Mlima TaboriHapa huenda ni mahali ambapo kugeuzwa kwa Yesu Kristo kulitokea. (33)

Picha
Bustani ya Gethsemane

Bustani ya GethsemaneYesu Kristo aliomba, aliteseka kwa ajili ya dhambi zetu, alisalitiwa na Yuda Iskariote, na alikamatwa katika bustani hii. (51, 52)

Picha
Golgotha

GolgothaHapa huenda pakawa mahali ambapo Yesu Kristo alikufa msalabani. (53)

Picha
Kaburi la Bustani.

Kaburi la BustaniHapa huenda ni mahali ambapo Yesu Kristo alizikwa, alifufuka, na kuzungumza na Mariamu Magdalene. (53, 54)

Chapisha