Sura ya 33
Kuonekana katika Utukufu: Kugeuzwa
Yesu aliwachukua Petro, Yakobo, na Yohana kwenye kilele cha mlima kusali.
Yesu alipokuwa akisali, utukufu wa Mungu ulikuja juu Yake. Uso wake uling’aa kama jua. Manabii wawili wa Agano la Kale walioitwa Musa na Eliya walimjia. Walizungumza kuhusu kifo na ufufuo Wake uliokuwa unakuja.
Mathayo 17:2–3; Marko 9:3–4; Luka 9:29–31 (ona rejeo chini ya ukurasa 31a)
Yesu alipokuwa akisali, Mitume walilala.
Walipoamka, waliona utukufu wa Yesu Kristo, Musa, na Eliya. Walisikia sauti ya Baba wa Mbinguni ikishuhudia, “Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa Naye, msikieni yeye.”
Mitume walikuwa na hofu na wakaanguka chini. Yesu aliwagusa na kuwaambia wasiwe na hofu. Walipotazama juu, wajumbe wa mbinguni walikuwa wameondoka. Yesu aliwaambia Mitume wasimwambie yeyote kile walichokuwa wamekiona hadi baada ya kufa Kwake na kufufuka.