Scripture Stories
Sura ya 47: Wanawali Kumi


Sura ya 47

Wanawali Kumi

Picha
wanawake wameshikilia taa za mafuta

Yesu alisimulia hadithi kuhusu wasichana kumi walioenda kwenye harusi. Walimngoja bwana harusi aje na kuwakaribisha ndani. Hawakujua ni saa ngapi angekuja.

Picha
wanawake wameshikilia taa za mafuta

Wanawake hao kumi walikuwa na taa za mafuta. Watano kati yao walikuwa na busara. Walikuwa wamebeba mafuta ya ziada.

Picha
mwanamke akitazama taa ya mafuta

Wanawake wengine watano walikuwa wapumbavu. Walikuwa tu na mafuta yaliyokuwa ndani ya taa zao.

Picha
wanawake wakiongeza mafuta kwenye taa

Bwana harusi hakuja kwa muda mrefu. Mafuta ndani ya taa yaliisha. Wanawake watano wenye busara walikuwa na mafuta ya ziada ya kuweka ndani ya taa zao. Wanawake watano wapumbavu walilazimika kwenda kununua mafuta ya ziada.

Picha
wanawake wamesimama na bwana harusi

Walipokuwa wameenda, bwana harusi alikuja. Aliwakaribisha wanawake watano wenye busara kwenye harusi.

Picha
wanawake wakigonga mlango

Wakati wanawake watano wapumbavu waliporejea, mlango ulikuwa umefungwa. Hawangeweza kuingia kwenye harusi.

Picha
Yesu akiwatokea watu

Yesu ni kama bwana harusi katika hadithi hii. Waumini wa Kanisa ni kama wale wanawake kumi. Yesu atakapokuja tena, baadhi ya waumini watakuwa tayari. Watakuwa wametii amri za Mungu. Wengine hawatakuwa tayari. Hawataweza kuwa na Mwokozi atakapokuja tena.

Chapisha