Scripture Stories
Sura ya 12: Harusi huko Kana


Sura ya 12

Harusi huko Kana

Picha
Mariamu akizungumza na Yesu

Yesu Kristo na wanafunzi Wake walihudhuria karamu ya harusi huko Kana. Mariamu, mama wa Yesu, alikuwa huko. Alimwambia Yesu kwamba hakukuwa na divai kwa ajili ya wageni.

Picha
Yesu akizungumza na Mariamu

Yesu alimheshimu na kumpenda mama Yake. Alimuuliza kile alichotaka Yeye afanye.

Yohana 2:4 (ona rejeo chini ya ukurasa 4a)

Picha
Yesu na Mariamu wakizungumza na watumishi

Mariamu aliwaambia watumishi kwenye harusi wafanya chochote ambacho Yesu aliwaambia wafanye.

Picha
watumishi wakijaza mitungi kwa maji

Yesu aliwaambia watumishi wajaze mitungi sita mikubwa ya mawe kwa maji. Kila mtungi ulijaa kati ya galoni 18 na 27 (lita 68 na 102). Kisha alibadilisha maji kuwa divai.

Picha
watumishi wakimimina divai kutoka kwenye mitungi

Aliwaambia watumishi watoe divai kutoka kwenye mitungi na wampatie mtawala wa karamu.

Picha
mtu akinywa divai

Mtawala wa karamu alishangazwa alipokunywa divai. Divai bora kwa kawaida ilitolewa mwanzoni mwa karamu. Lakini wakati huu, divai bora ilitolewa mwisho.

Picha
Yesu na Mariamu

Huu ni muujiza wa kwanza kuwekwa kumbukumbu ambao Yesu alifanya wakati wa maisha yake duniani. Aliufanya ili kumsaidia mama Yake. Ulisaidia pia kuimarisha imani ya wanafunzi Wake.

Chapisha