Scripture Stories
Sura ya 41: Yesu Anawabariki Watoto


Sura ya 41

Yesu Anawabariki Watoto

Picha
watu wakiwaleta watoto kwa Yesu

Yesu alikuwa akienda Yerusalemu. Njiani baadhi ya watu walimtaka Yesu awabariki watoto wao. Wanafunzi waliwaambia watu wasimsumbue Yesu.

Picha
Yesu akiwabariki watoto

Lakini Yesu Kristo anawapenda watoto. Aliwaambia wanafunzi wawaache watoto waje Kwake. Yesu pia aliwaambia wanafunzi kwamba wanapaswa kuwa kama watoto wadogo. Kisha wataweza kuishi pamoja na Mungu mbinguni.

Chapisha