Sura ya 41
Yesu Anawabariki Watoto
Picha
watu wakiwaleta watoto kwa Yesu
Yesu alikuwa akienda Yerusalemu. Njiani baadhi ya watu walimtaka Yesu awabariki watoto wao. Wanafunzi waliwaambia watu wasimsumbue Yesu.
Picha
Yesu akiwabariki watoto
Lakini Yesu Kristo anawapenda watoto. Aliwaambia wanafunzi wawaache watoto waje Kwake. Yesu pia aliwaambia wanafunzi kwamba wanapaswa kuwa kama watoto wadogo. Kisha wataweza kuishi pamoja na Mungu mbinguni.