Scripture Stories
Sura ya 43: Yesu Anamfufua Lazaro


Sura ya 43

Yesu Anamfufua Lazaro

Picha
Yesu akila pamoja na Mariamu, Martha, na Lazaro

Mtu aliyeitwa Lazaro aliishi Bethania na dada zake Mariamu na Martha. Yesu alimpenda Lazaro na dada zake, na wao walimpenda Yesu.

Picha
Lazaro mgonjwa amelala kitandani

Lazaro akawa mgonjwa sana. Mwokozi alikuwa katika mji mwingine. Mariamu na Martha walituma ujumbe Kwake kwamba Lazaro alikuwa mgonjwa.

Picha
mtu akizungumza na Yesu

Mwokozi aliwaambia wanafunzi Wake waende Naye kumsaidia Lazaro. Wanafunzi walikuwa na hofu kwenda Bethania. Ilikuwa karibu na Yerusalemu. Baadhi ya watu huko Yerusalemu walitaka kumwua Yesu.

Picha
Yesu na wanafunzi wakisafiri

Yesu aliwaambia wanafunzi Wake kwamba Lazaro alikuwa amekufa. Alisema kwamba Yeye angemfufua. Muujiza huu ungewasaidia wanafunzi kujua kwamba Yeye alikuwa Mwokozi. Yesu alienda Bethania. Alipofika huko, Lazaro alikuwa amekufa kwa siku nne.

Picha
Yesu akizungumza na Martha

Martha alimwambia Yesu kwamba Lazaro angelikuwa bado hai kama Yeye angelikuja mapema. Yesu alisema Lazaro angeishi tena. Alimuuliza Martha kama alimuamini. Martha alisema ndio. Alijua kwamba Yesu alikuwa Mwokozi.

Picha
Mariamu akilia miguuni pa Yesu

Martha alimuacha Yesu na kwenda kumwita dada yake, Mariamu. Mariamu alienda kukutana na Yesu pia. Watu wengi walimfuata. Mariamu alipiga magoti, akilia, miguuni pa Mwokozi. Watu waliokuwa naye walikuwa wakilia pia. Yesu aliuliza mahali mwili wa Lazaro ulipokuwa.

Picha
watu wakisogeza jiwe kutoka kwenye mlango wa kaburi

Yesu alienda kwenye pango ambamo Lazaro alikuwa amezikwa. Kulikuwa na jiwe mbele yake. Aliwaambia watu wasogeze jiwe.

Picha
Yesu akitazama juu

Yesu alitazama juu. Alimshukuru Baba wa Mbinguni kwa kusikiliza maombi Yake.

Picha
Lazaro akitembea kumwelekea Yesu

Kisha, kwa sauti kubwa, Yesu alimwambia Lazaro atoke pangoni. Lazaro alitoka nje. Watu wengi walioona muujiza huo sasa waliamini kwamba Yesu alikuwa Mwokozi.

Chapisha