Sura ya 59
Sauli Anajifunza kuhusu Yesu
Sauli alikuwa amewaona watu wakimwua Stefano. Siku moja Sauli alikuwa akitembea kuelekea mji wa Dameski na marafiki kadhaa. Alikuwa akitaka kuwaweka baadhi ya wanafunzi wa Kristo gerezani.
Ghafla mwangaza mkali uliong’aa kutoka mbinguni ulimzingira. Alianguka chini. Kisha Sauli alisikia sauti ya Yesu ikimuuliza ni kwa nini alikuwa akijaribu kuwadhuru Watakatifu. Sauli aliogopa. Alimuuliza Yesu kile alichopaswa kufanya. Mwokozi alisema Sauli alipaswa kwenda Dameski. Huko Sauli angeambiwa kile alichohitajika kufanya.
Sauli alifungua macho yake, lakini hakuweza kuona. Alikuwa kipofu. Rafiki zake walimpeleka Dameski.
Mwanafunzi wa Yesu Kristo aliyeitwa Anania aliishi Dameski. Katika ono, Yesu alimwambia Anania aende kwa Sauli.
Anania alikuwa na ukuhani. Aliweka mikono yake juu ya kichwa cha Sauli na kumbariki kwamba macho ya Sauli yangepata kuona. Baada ya kuponywa, Sauli alibatizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Sauli alibadilisha jina lake kuwa Paulo. Aliitwa kuwa Mtume. Alikuwa mmisionari wa Kanisa. Aliandika barua nyingi. Alikwenda kwenye nchi nyingi na alifundisha injili.