Scripture Stories
Fumbo la Kwanza: Kondoo Aliyepotea


Fumbo la Kwanza

Kondoo Aliyepotea

Picha
mchungaji na kondoo

Mchungaji mwema alikuwa na kondoo 100. Mmoja wao alikuwa amepotea.

Picha
mchungaji akimtafuta kondoo aliyepotea

Mchungaji aliwaacha wale kondoo 99 kumtafuta yule mmoja aliyepotea. Alipompata, alikuwa na furaha sana.

Picha
mchungaji amembeba kondoo

Mchungaji alimbeba kondoo kumleta nyumbani. Aliwaita rafiki zake wote na majirani waje na kufurahia pamoja naye. Alikuwa amempata kondoo aliyepotea.

Picha
Yesu amesimama

Yesu Kristo aliwaambia Mafarisayo kile ambacho fumbo lilimaanisha. Alisema kwamba wale wanaotenda dhambi ni kama kondoo aliyepotea.

Picha
Yesu akinyoosha mkono

Kama vile mchungaji alivyotaka kumuokoa kondoo aliyepotea, Yesu anataka kuwaokoa wale wanaotenda dhambi.

Picha
Yesu amesimama na mtu

Yesu alisema kwamba hiyo ndiyo sababu alikuwa akizungumza na wenye dhambi.

Mathayo 18:11 (ona rejeo chini ya ukurasa 11c); Marko 2:17

Picha
Yesu amesimama pamoja na mwanaume na mwanamke

Na kama vile mchungaji alivyokuwa na furaha alipompata kondoo aliyepotea, Yesu hufurahia pale tunapotubu.

Chapisha