Scripture Stories
Sura ya 61: Paulo na Sila Gerezani


Sura ya 61

Paulo na Sila Gerezani

Picha
msichana amekaa na mikono ikiwa kichwani

Msichana alikuwa na pepo ndani yake. Watu walipenda kusikiliza kile pepo lilisema kupitia yeye. Waliwalipa watu ambao msichana aliwafanyia kazi ili kusikia pepo likizungumza.

Picha
watu wakizungumza na msichana

Wakati wowote Paulo na Sila walipopita, msichana yule aliwafuata. Alipokuwa akifanya hivyo, pepo lilizungumza. Siku moja Paulo aliliamuru pepo limtoke. Lilimtoka. Watu ambao msichana aliwafanyia kazi walikasirika. Sasa wasingeweza kupata pesa.

Picha
watu wakiwapigia kelele Mitume

Watu waliwapeleka Paulo na Sila kwa viongozi wa mji. Walisema kwamba Paulo na Sila walikuwa wakisababisha matatizo.

Picha
askari wakiwapiga mijeledi Mitume

Viongozi waliwafanya Paulo na Sila wapigwe mijeledi na kutupwa gerezani.

Picha
Mitume wakiomba

Usiku ule Paulo na Sila waliomba na kuimba nyimbo kwa Baba wa Mbinguni. Watu wote gerezani waliwasikia. Ghafla ardhi ilianza kutetemeka. Milango ya gereza ikafunguka.

Picha
Mitume wakizungumza na mlinzi

Mlinzi aliamka na kuona milango iko wazi. Alifikiri wafungwa walikuwa wametoroka. Paulo alimwambia mlinzi asiwe na shaka. Wafungwa walikuwa wote bado wako pale. Mlinzi alipiga magoti kando ya Paulo na Sila na kuuliza jinsi anavyoweza kuokoka.

Picha
Mtume akimbatiza mlinzi

Paulo na Sila walimfundisha mlinzi na familia yake injili. Usiku ule mlinzi na familia yake walibatizwa.

Picha
askari wakiwapungia mkono Mitume

Siku iliyofuata viongozi wa mji waliwaachilia Paulo na Sila. Paulo na Sila walienda mji mwingine kufanya kazi zaidi ya umisionari.

Chapisha