Sura ya 61
Paulo na Sila Gerezani
Wakati wowote Paulo na Sila walipopita, msichana yule aliwafuata. Alipokuwa akifanya hivyo, pepo lilizungumza. Siku moja Paulo aliliamuru pepo limtoke. Lilimtoka. Watu ambao msichana aliwafanyia kazi walikasirika. Sasa wasingeweza kupata pesa.
Watu waliwapeleka Paulo na Sila kwa viongozi wa mji. Walisema kwamba Paulo na Sila walikuwa wakisababisha matatizo.
Viongozi waliwafanya Paulo na Sila wapigwe mijeledi na kutupwa gerezani.
Usiku ule Paulo na Sila waliomba na kuimba nyimbo kwa Baba wa Mbinguni. Watu wote gerezani waliwasikia. Ghafla ardhi ilianza kutetemeka. Milango ya gereza ikafunguka.
Mlinzi aliamka na kuona milango iko wazi. Alifikiri wafungwa walikuwa wametoroka. Paulo alimwambia mlinzi asiwe na shaka. Wafungwa walikuwa wote bado wako pale. Mlinzi alipiga magoti kando ya Paulo na Sila na kuuliza jinsi anavyoweza kuokoka.
Paulo na Sila walimfundisha mlinzi na familia yake injili. Usiku ule mlinzi na familia yake walibatizwa.
Siku iliyofuata viongozi wa mji waliwaachilia Paulo na Sila. Paulo na Sila walienda mji mwingine kufanya kazi zaidi ya umisionari.