Scripture Stories
Sura ya 19: Mahubiri ya Mlimani


Sura ya 19

Mahubiri ya Mlimani

Picha
Yesu akiwafundisha wanafunzi

Siku moja Yesu aliwafundisha wanafunzi Wake injili kwenye upande wa mlima kando ya Bahari ya Galilaya.

Picha
Yesu akiwafundisha wanafunzi

Aliwaambia jinsi ya kuishi ili waweze kuwa na furaha na kuishi na Baba wa Mbinguni tena. Vitu alivyowafundisha vinaweza kutufanya tuwe na furaha pia.

Picha
Yesu akifundisha

Yesu alisema tunapaswa tuwe wapole, wavumilivu, na tayari kumtii Baba wa Mbinguni.

Picha
Yesu akiwafundisha wanafunzi

Tunapaswa tujaribu kadri tuwezavyo kuwa waadilifu.

Picha
mtu akimuumiza mwenzake

Tunapaswa tuwasamehe watu wanaotuumiza ama kutufanya tuhisi vibaya. Tukiwasamehe, Baba wa Mbinguni atatusamehe.

Picha
Wanandoa wakishiriki na wengine chakula

Tunapaswa tuwe wapatanishi, tuwapende watu wengine, na kusaidia kila mmoja kupendana.

Picha
mwanaume akizungumza na mwanamke

Hatupaswi kuwa waoga kuwaambia watu kuhusu injili au kuwaonyesha kwamba tunampenda Baba wa Mbinguni. Watu wengine wanapotuona tukifanya mema, itawasaidia kumwamini Mungu pia.

Picha
mwanaume akimpa pesa mwanamke

Tunapaswa daima tutimize ahadi zetu.

Picha
Mwanaume akimsaidia mwanaume mwingine

Na kama vile tunavyotaka wengine wawe wema kwetu, tunapaswa tuwe wema kwao.

Picha
Yesu akiwafundisha watu

Yesu alisema kwamba ikiwa tutafanya vitu hivi, tutakuwa na furaha, Baba wa Mbinguni atatubariki, na tutaishi Naye tena.

Chapisha