Scripture Stories
Sura ya 34: Mvulana mwenye Pepo mchafu


Sura ya 34

Mvulana mwenye Pepo mchafu

Picha
mtu akizungumza na Yesu

Siku moja mtu alimsihi Mwokozi amsaidie mwanawe. Mvulana alikuwa na pepo mchafu ndani yake. Wanafunzi walikuwa wameshajaribu kumponya mwanawe, lakini hawakuweza.

Picha
mvulana amelala chini ardhini

Yesu alimwambia mtu yule amlete mwanawe Kwake. Mvulana alipokuja, pepo mchafu lilimfanya aanguke chini.

Picha
Yesu akizungumza na mtu

Mwokozi aliuliza pepo lilikuwa ndani ya mvulana kwa muda gani. Baba alisema kwamba lilikuwa limekuwa ndani yake tangu alipokuwa mtoto.

Picha
mtu akilia

Yesu alisema angemponya mwanae kama baba angekuwa na imani. Baba alianza kulia. Alisema kwamba alikuwa na imani. Lakini alimsihi Yesu amsaidie awe na imani zaidi.

Picha
Yesu akimponya mvulana

Yesu aliliamuru pepo limtoke mvulana na kamwe lisimuingie tena. Pepo lilikasirika. Lilimuumiza mvulana tena. Kisha lilimtii Yesu na kutoka.

Picha
Yesu akimsaidia mvulana kusimama

Mvulana alikuwa kimya sana kiasi kwamba watu walisema alikuwa amekufa. Lakini Yesu alichukua mkono wake na kumsaidia kusimama. Mvulana alikuwa ameponywa. Pepo lilikuwa limeondoka.

Picha
Yesu akifundisha wanafunzi

Baadaye wanafunzi walimuliza Yesu ni kwa nini hawakuweza kulifanya pepo limtoke mvulana. Yesu aliwaambia kwamba wakati mwingine walihitaji kufunga na kusali ili mtu aweze kuponywa.

Chapisha