Sura ya 34
Mvulana mwenye Pepo mchafu
Siku moja mtu alimsihi Mwokozi amsaidie mwanawe. Mvulana alikuwa na pepo mchafu ndani yake. Wanafunzi walikuwa wameshajaribu kumponya mwanawe, lakini hawakuweza.
Yesu alimwambia mtu yule amlete mwanawe Kwake. Mvulana alipokuja, pepo mchafu lilimfanya aanguke chini.
Mwokozi aliuliza pepo lilikuwa ndani ya mvulana kwa muda gani. Baba alisema kwamba lilikuwa limekuwa ndani yake tangu alipokuwa mtoto.
Yesu alisema angemponya mwanae kama baba angekuwa na imani. Baba alianza kulia. Alisema kwamba alikuwa na imani. Lakini alimsihi Yesu amsaidie awe na imani zaidi.
Yesu aliliamuru pepo limtoke mvulana na kamwe lisimuingie tena. Pepo lilikasirika. Lilimuumiza mvulana tena. Kisha lilimtii Yesu na kutoka.
Mvulana alikuwa kimya sana kiasi kwamba watu walisema alikuwa amekufa. Lakini Yesu alichukua mkono wake na kumsaidia kusimama. Mvulana alikuwa ameponywa. Pepo lilikuwa limeondoka.
Baadaye wanafunzi walimuliza Yesu ni kwa nini hawakuweza kulifanya pepo limtoke mvulana. Yesu aliwaambia kwamba wakati mwingine walihitaji kufunga na kusali ili mtu aweze kuponywa.