Sura ya 29
Yesu Anatembea Juu ya Maji
Baada ya kuwalisha wale 5,000, Yesu alienda juu mlimani kusali. Wanafunzi wake walichukua mashua ili kuvuka Bahari ya Galilaya. Usiku ulipofika, upepo ulianza kuvuma, na mawimbi yakapanda.
Baadaye usiku sana, Yesu alikuja kuungana na wanafunzi Wake. Alikuwa akitembea juu ya maji kwenda kwenye mashua.
Wanafunzi walimuona akiwa anatembea juu ya maji. Waliogopa. Walifikiri alikuwa pepo. Yesu aliwaita, “Ni Mimi; msiogope.”
Petro alitaka kutembea juu ya maji pia. Yesu alimwambia Petro aje Kwake. Petro alishuka kutoka kwenye mashua. Alianza kutembea juu ya maji kuelekea kwa Mwokozi.
Kwa sababu upepo ulikuwa unavuma sana, Petro alishikwa na hofu. Alianza kuzama majini na akapiga kelele kwa Yesu amwokoe.
Mwokozi alishika mkono wa Petro. Alimwuliza Petro kwa nini hakuwa na imani zaidi.
Wakati Yesu na Petro walipokuja kwenye mashua, tufani ilikoma. Wanafunzi wote walimuabudu Mwokozi. Walijua kwamba alikuwa Mwana wa Mungu.