Watu wa Kujua
- Agripa
-
mfalme wa Kirumi aliyetawala Israeli. Paulo alimwambia Agripa huhusu Yesu Kristo.
- Ana
-
mjane mwaminifu ambaye alimwona Yesu akiwa mtoto na kuwafundisha watu kwamba Yesu alikuwa Mwana wa Mungu na Mkombozi
- Anania
-
mwanafunzi wa Yesu Kristo aliyeishi Dameski. Alimbariki Paulo na kumhudumia baada ya Paulo kupofushwa wakati wa ono.
- Baba wa Mbinguni
-
Baba wa miili yetu ya kiroho. Sisi tunaomba Kwake.
- Elisabeti
-
mama yake Yohana Mbatizaji
- Eliya
-
nabii wa Agano la Kale
- Gabrieli
-
malaika ambaye alimtembelea Mariamu na kumwambia kwamba angekuwa mama wa Yesu. Gabrieli pia alimjia Zakaria na kumwambia angekuwa na mwana ambaye angekuwa Yohana Mbatizaji.
- Herode
-
mfalme mwovu aliyetawala Yerusalemu wakati Yesu alipozaliwa. Aliwaua watoto wote Bethlehemu kwa matumaini ya kumwua mtoto Yesu.
- Isaya
-
nabii wa Agano la Kale ambaye aliandika kuhusu Yesu
- Joseph Smith
-
Joseph Smith alipokuwa kijana, Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo walimtembelea. Walimwambia asijiunge na mojawapo ya makanisa ambayo yalikuwa duniani kwa sababu yote yalikuwa yamepotoka kutoka kwenye ukweli. Kupitia Joseph Smith, Kanisa la ukweli la Yesu Kristo lilirejeshwa duniani.
- Kayafa
-
kuhani mkuu Myahudi ambaye alishiriki katika kumtia hatiani Yesu kwenye kushitakiwa Kwake
- Lazaro
-
mtu ambaye Yesu alimfufua
- Mafarisayo
-
viongozi wa Wayahudi. Wengi wao walimchukia Yesu na wanafunzi Wake.
- Mariamu
-
mama yake Yesu
- Mariamu and Martha
-
dada zake Lazaro na marafiki wa Yesu
- Mariamu Magdalene
-
Rafiki wa Yesu na mtu wa kwanza kumwona Yesu baada ya Ufufuko Wake
- Masiya
-
jina lingine la Yesu Kristo
- Mathiya
-
mwanafunzi wa Yesu ambaye aliitwa kuchukua nafasi ya Yuda Iskariote kama mmoja wa Mitume Kumi na Wawili
- Mungu
-
linaweza kuhusu Baba wa Mbinguni ama Yesu Kristo
- Musa
-
nabii wa Agano la Kale
- Mwokozi
-
Yesu Kristo ndiye Mwokozi. Aliteseka na kufa kwa ajili ya dhambi zetu. Kwa sababu Yake, tunaweza kusamehewa dhambi zetu, kama tukitubu, na tutaishi milele.
- Nikodemo
-
mtawala wa Wayahudi ambaye aliamini kwamba Yesu alikuwa Mwokozi. Yesu alimfundisha Nikodemo kuhusu ubatizo.
- Paulo
-
mtu ambaye hakuwapenda wanafunzi wa Yesu hadi alipomwona Yesu katika ono na kuongoka. Kisha alimtumikia Mungu na kuwa mmoja wa Mitume. Alijulikana pia kama Sauli.
- Petro
-
mmoja wa Mitume Kumi na Wawili wa Yesu na Rais wa Kanisa baada ya kifo cha Yesu
- Pontio Pilato
-
gavana Mrumi katika Yerusalemu. Wayahudi walimwambia Pilato amsulubishe Yesu, na Pilato alikubali Yesu kuuawa.
- Roho Mtakatifu
-
mmoja wa washiriki watatu wa Uungu. Huwasaidia Yesu Kristo na Baba wa Mbinguni. Ana uwezo wa kusaidia watu kujua ukweli. Yeye ni roho na hana mwili wa nyama na mfupa.
- Sauli
-
ona Paulo
- Shetani
-
mwana wa kiroho wa Baba wa Mbinguni. Hakumtii Baba wa Mbinguni, hivyo alifukuzwa mbinguni. Akawa ibilisi. Shetani hujaribu kushawishi watu kufanya yale ambayo ni maovu.
- Sila
-
mmisionari na rafiki wa Paulo
- Simioni
-
mtu mwadilifu ambaye alimwona mtoto Yesu hekaluni huko Yerusalemu
- Simoni
-
mtu katika Samaria. Alijaribu kununua ukuhani kutoka kwa Petro na Yohana. Walimfundisha kwamba mtu hawezi kununua ukuhani.
- Stefano
-
kiongozi mwadilifu wa Kanisa la Yesu Kristo. Mafarisayo walimwua.
- Tabitha
-
mwanamke mwema ambaye Petro alimfufua
- Warumi
-
watu waliodhibiti nchi ambayo Yesu aliishi wakati wa maisha Yake
- Wasamaria
-
Kundi la watu ambao waliishi katika nchi ambayo Yesu aliishi. Wayahudi na Wasamaria kwa kawaida hawakupendana.
- Wayahudi
-
Waisraeli ambao walikuwa sehemu ya ufalme wa Yuda. Yesu alikuwa Myahudi.
- Yairo
-
kiongozi Myahudi katika Kapernaumu. Yesu alimfufua binti yake.
- Yakobo
-
mmoja wa Mitume Kumi na Wawili wa Yesu. Alikuwa mmoja wa washauri wa Petro baada ya kifo cha Yesu.
- Yesu Kristo
-
Mwana wa Mungu na Mwokozi wa ulimwengu. Aliteseka na kufa kwa ajili ya dhambi zetu.
- Yohana
-
mmoja wa Mitume Kumi na Wawili wa Yesu. Alikuwa mmoja wa washauri wa Petro baada ya kifo cha Yesu.
- Yohana Mbatizaji
-
nabii aliyembatiza Yesu. Alikuwa mwana wa Zakaria na Elisabeti.
- Yuda Iskariote
-
mmoja wa Mitume wa Yesu. Yuda alimsaliti Yesu kwa watu waovu kwa vipande 30 vya fedha.
- Yusufu
-
Mume wa Mariamu. Yusufu aliwatunza vyema Yesu na Mariamu.
- Zakaria
-
baba yake Yohana Mbatizaji