Sura ya 7
Mamajusi
Picha
mamajusi wakiiona nyota mpya
Mamajusi fulani waliishi katika nchi nyingine. Walijua kile ambacho manabii walikuwa wamesema kuhusu kuzaliwa kwa Yesu. Walipoiona nyota mpya angani, walijua kwamba mfalme mpya alikuwa amezaliwa.
Picha
mamajusi wakizungumza na Mfalme Herode
Mamajusi walienda kumwona Herode, mfalme wa Wayahudi, huko Yerusalemu. Walimuuliza wapi mfalme mpya alipokuwa. Herode aliwaambia wakatafute Bethlehemu. Watakapompata mtoto wangerudi na kumwambia Herode.
Picha
mamajusi wakimtembelea mtoto Yesu
Mamajusi walienda Bethlehemu na kumpata Yesu. Walimwabudu na kumpa zawadi. Waliambiwa katika ndoto wasirudi Yerusalemu na kumwambia Herode wapi alipo mtoto. Hawakurudi.