Scripture Stories
Sura ya 32: Petro Anashuhudia juu ya Kristo


Sura ya 32

Petro Anashuhudia juu ya Kristo

Picha
Yesu akiwafundisha wanafunzi

Yesu aliwauliza wanafunzi Wake watu walidhani Yeye ni nani.

Picha
wanafunzi wakizungumza na Yesu

Wanafunzi walijibu kwamba baadhi ya watu walidhani Yesu alikuwa Yohana Mbatizaji. Wengine walidhani alikuwa nabii wa Agano la Kale aliyekuwa amefufuka.

Picha
Petro akizungumza

Yesu aliwauliza wanafunzi Wake walidhani Yeye alikuwa ni nani. Petro alisema, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”

Picha
Yesu akizungumza na wanafunzi

Yesu alieleza kwamba ushuhuda wa Petro haukuja kutoka kwa mafundisho ya watu. Ushuhuda wake ulikuwa umekuja kwa ufunuo kutoka kwa Mungu.

Picha
Yesu akizungumza na Petro

Yesu alimwahidi Petro kwamba angempa ukuhani na mamlaka ya kuongoza Kanisa Lake. Kisha Petro na wanafunzi wangekuwa na mamlaka ya kuanzisha Kanisa la Yesu duniani.

Picha
Yesu amesimama kando ya Petro

Yesu aliwaambia wanafunzi Wake wasimwabie yeyote kwanza kwamba Yeye alikuwa ndiye Kristo. Kwanza alihitaji kuteseka, kuuwawa, na kufufuka siku ya tatu.

Chapisha