Sura ya 32
Petro Anashuhudia juu ya Kristo
Yesu aliwauliza wanafunzi Wake watu walidhani Yeye ni nani.
Wanafunzi walijibu kwamba baadhi ya watu walidhani Yesu alikuwa Yohana Mbatizaji. Wengine walidhani alikuwa nabii wa Agano la Kale aliyekuwa amefufuka.
Yesu aliwauliza wanafunzi Wake walidhani Yeye alikuwa ni nani. Petro alisema, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
Yesu alieleza kwamba ushuhuda wa Petro haukuja kutoka kwa mafundisho ya watu. Ushuhuda wake ulikuwa umekuja kwa ufunuo kutoka kwa Mungu.
Yesu alimwahidi Petro kwamba angempa ukuhani na mamlaka ya kuongoza Kanisa Lake. Kisha Petro na wanafunzi wangekuwa na mamlaka ya kuanzisha Kanisa la Yesu duniani.
Yesu aliwaambia wanafunzi Wake wasimwabie yeyote kwanza kwamba Yeye alikuwa ndiye Kristo. Kwanza alihitaji kuteseka, kuuwawa, na kufufuka siku ya tatu.