Scripture Stories
Yaliyomo


Yaliyomo

Vyanzo

Baadhi ya taarifa katika kitabu hiki zimetolewa kutoka kwenye vyanzo visivyo vya kimaandiko vilivyodondolewa hapa chini.

Kamusi ya Biblia katika toleo la Watakatifu wa Siku za Mwisho la Biblia ya King James (1979)

James E. Talmage, Jesus the Christ, toleo la 3 (1916)

Mafundisho ya Nabii Joseph Smith, sel. Joseph Fielding Smith (1976)

Kwa Msomaji

Hadithi za Agano Jipya zimeandikwa mahususi kwa ajili yako. Hadithi hizi zimetolewa kutoka kwenye kitabu ambacho ni kitakatifu. Unaposoma hadithi hizi, kumbuka kuwa zinawahusu watu wa kweli ambao waliishi hapo zamani za kale.

Zisome hadithi tena na tena hadi uzijue vyema. Utataka pia kuzisoma kutoka kwenye Biblia. Chini ya picha nyingi, utaona marejeo yanayokuambia wapi utapata hadithi hiyo katika Biblia au vitabu vingine. Acha baba yako, mama, mwalimu, ama rafiki akusaidie kupata hadithi katika maandiko.

Kama haujui nini maana ya neno, litafute katika sehemu ya “Maneno ya Kujua” mwishoni mwa kitabu. Kama unataka kujifunza zaidi kuhusu sehemu, itafute katika sehemu ya “Sehemu za Kujua.” Kama haumjui mtu ni nani, mtafute katika sehemu ya “Watu wa Kujua.” Hiki kitabu pia kina sehemu ambayo ina picha za mahali katika Nchi Takatifu na mpangilio wa muda wa Agano Jipya.

Kwa Wazazi na Walimu

Kitabu hiki kinaweza kusaidia kufundisha maandiko. Tumia sehemu za “Maneno ya Kujua,” “Sehemu za Kujua,” na “Watu wa Kujua” ili kuwasaidia watoto wawe na mazoea ya maneno, watu na sehemu katika kitabu hiki. Nyenzo zingine saidizi katika kitabu hiki zinajumuisha ramani, picha, na mfululizo wa muda.

Unapofundisha, shiriki ushuhuda wako wa Biblia. Wahimize wale unaowafundisha watafute kwa maombi ushuhuda wao wenyewe wa maandiko na wa Mwokozi, Yesu Kristo. Uelewa wa wale unaowafundisha utakua zaidi unapowasomea hadithi wanazozipenda kutoka kwenye Biblia yenyewe.

Chapisha