Maneno ya Kujua
- abudu
-
kumsifu, kumpenda na kumtii Mungu
- adilifu
-
utiifu kwa amri za Mungu
- ahadi
-
kusema utafanya kitu
- amini
-
kuhisi kwamba jambo fulani ni sahihi ama la kweli
- amri
-
kitu ambacho Mungu huwaambia watu wafanye ili wawe na furaha
- amrisha
-
kumwambia mtu ama kitu nini cha kufanya
- anzisha
-
kuweka katika utaratibu Kanisa la Yesu Kristo
- askari
-
mtu ambaye hutekeleza maagizo ya mfalme ama kiongozi
- baraka
-
sala maalumu kumuomba Baba wa Mbinguni kumfariji au kumponya mtu; mtu anayetoa sala hii hufanya hivyo kwa nguvu ya ukuhani ambao anao. Usaidizi wowote tunaopata kutoka kwa Mungu.
- bariki
-
kutoa vitu vizuri au kumsaidia mtu
- boflo [maboflo]
-
umbo ambao mkate huokwa
Pichaboflo - busara
-
mtu ambaye ana maarifa mengi na anaelewa watu, sheria na maandiko; pia mtu ambaye hupanga kwa ajili ya siku za usoni
- bwana harusi
-
mwanaume ambaye anaoa
- chagua
-
kuchukua ama kuteua
- daima
-
kila mara
- danganya
-
kutosema ukweli
- dhabihu
-
kutoka kitu cha maana kwa ajili ya Mungu ama watu wengine
- dhambi
-
kutotii amri za Baba wa Mbinguni
- divai
-
kinywaji kilichotengenezwa kwa zabibu
- fuata
-
kufanya kile ambacho mtu mwingine anafanya
- fufuka
-
kuwa na miili yetu na roho kurudiana pamoja baada ya kufa kwetu
- fumbo
-
hadithi ambayo hufundisha kanuni au somo
- gereza
-
mahali ambapo watu waliovunja sheria huwekwa
- harusi
-
tukio ambapo mwanaume na mwanamke huoana
- hekalu
-
nyumba ya Mungu duniani; mahali pa kumwabudu Mungu; mahali patakatifu ambapo ibada takatifu hufanywa
Pichahekalu - hori
-
sanduku ambamo chakula huwekwa kwa ajili ya wanyama kula
Pichahori - iba
-
kuchukua kitu ambacho ni cha mtu mwingine
- ibilisi
-
jina lingine la Shetani
- imani
-
kuamini na kutumaini katika Yesu Kristo
- inama [aliinama]
-
kuinamisha kichwa chini kwa heshima
Pichakuinamisha kichwa - injili
-
mafundisho ya Yesu Kristo kuhusu jinsi watu wanavyopaswa kuishi ili kwamba waweze kurudi na kuishi na Baba wa Mbinguni; ni mpango wa wokovu wa Baba wa Mbinguni
- jangwa
-
nchi ambayo ina maji kidogo sana na mimea michache au wanyama
- jaribu
-
kujaribu kufanya mtu afanye kitu ambacho ni kibaya
- jeraha
-
dhara baya mwilini kwa mtu
- jirani
-
mtu anayeishi karibu na nyumba yako; mtoto yeyote wa Mungu
- jiunge
-
kuwa sehemu ya kundi
- joho
-
kipande cha nguo kilicho kirefu, na kinachoburuza chini ambacho huvaliwa juu ya nguo nyingine
Pichajoho - kaburi
-
mahali ambapo watu waliokufa huzikwa
Pichakaburi - karamu
-
mlo mkubwa ambao kwa kawaida huliwa siku maalumu
- kejeli
-
kudhihaki
- kidonda
-
sehemu mwilini ambayo inauma ama kuvuja damu
- kiongozi
-
mtu anayeelekeza na anawajibika kwa ajili ya kundi la watu
- kipawa cha Roho Mtakatifu
-
haki ya kuwa na usaidizi wa Roho Mtakatifu; hupewa mtu baada ya ubatizo na mtu aliye na mamlaka ya ukuhani
- kipofu
-
kutoweza kuona
- kiziwi
-
kutoweza kusikia
- kufunga
-
kuacha kula chakula na maji unapotafuta baraka kutoka kwa Baba wa Mbinguni
- kugeuzwa
-
badiliko kwa mtu kwa muda mfupi ambalo hufanya aweze kuwa katika uwepo wa Baba wa Mbinguni
- kuhani
-
kiongozi katika kanisa
- kujazwa na Roho Mtakatifu
-
Kuwa na Roho Mtakatifu kujaza akili na moyo wa mtu kwa ukweli
- maandiko
-
vitabu ambavyo vina maneno ya Mungu yanayotolewa kupitia manabii Wake
- madhabahu
-
muundo mtukufu unaofanana na meza hekaluni wakati Yesu alipokuwa hai. Watu walitoa dhabihu kwa Mungu juu ya madhabahu.
Pichamadhabahu - mahubiri
-
Mazungumzo yanayotolewa kwa kundi la watu kuhusu injili
- Malaika
-
mjumbe wa mbinguni kutoka kwa Mungu
- Mamajusi
-
wanaume ambao walikuja kutoka Mashariki kumtembelea Yesu alipokuwa mtoto mchanga
- mamlaka
-
haki ya kutumia nguvu kama vile ukuhani au kuwa na haki ya kuwaadhibu wale ambao hawatii sheria
- mbinguni
-
mahali ambapo Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaishi
- mchungaji
-
mtu anayewatunza kondoo
Pichamchungaji - milele
-
kitu ambacho hakina mwisho; kinaendelea milele
- misheni
-
wakati maalumu wa kwenda kuhudumu na kufundisha watu injili ya Yesu Kristo na kuimarisha ufalme wa Mungu duniani
- mjane
-
mwanamke ambaye mumewe amekufa
- mjeledi
-
uzi au kamba nyembamba; kutumia mjeledi kupiga mtu ama kitu
Pichamjeledi - mkoma
-
mtu mgonjwa mwenye vidonda mwili mzima
- mlima
-
mlima ama kilima kikubwa
- mlinzi
-
mtu anayewaangalia watu gerezani; kuangalia watu, sehemu, ama kitu
- mmisionari
-
mtu ambaye huenda misheni; wakati mwingine mtu huyo huitwa kwenda nchi zingine
- mpatanishi
-
mtu anayewasaidia watu wasikasirikiane
- mshauri
-
mtu anayesaidia ama kutoa nasaha kwa mtu mwingine
- Mtakatifu
-
muumini wa Kanisa la kweli la Yesu Kristo
- Mtume
-
kiongozi katika Kanisa la Yesu Kristo ambaye humshuhudia Yesu Kristo na kufundisha injili
- mtumwa
-
mtu anayehudumu au kumfanyia kazi mtu mwingine au Mungu
- muujiza
-
kitu kisicho cha kawaida ambacho hutokea kwa sababu ya nguvu za Mungu
- muumini
-
mtu ambaye yuko katika kanisa ama kikundi kingine
- mvivu
-
kutokuwa tayari kufanya kazi
- mwanafunzi
-
mtu anayeamini katika Yesu Kristo na anayejaribu kuwa kama Yeye
- mwenye dhambi
-
mtu ambaye hatii amri za Baba wa Mbinguni
- mwenye nyumba ya wageni
-
mtu ambaye anamiliki nyumba ya wageni
- mwiba
-
sehemu kali na yenye ncha ya mmea ambayo inaweza kuumiza ikiguswa
- mwili wa nyama na damu
-
miili ambayo watu duniani wanayo ambayo imeundwa kwa ngozi, mifupa, misuli, na damu
- mwizi [wezi]
-
mtu ambaye huiba kutoka kwa wengine
- mwovu
-
mtu ambaye ni mwovu
- mzabibu
-
shina kuu la mmea, kama vile zabibu, ambalo lina matawi yanayozunguka yatokanayo na mmea huo. mzabibu huyaweka matawi hai
Pichamzabibu - nabii
-
mtu aliyeitwa na Mungu kuwaambia watu kile Mungu anawataka wafanye
- nguvu
-
uwezo wa kufanya kitu fulani. Pia ona ukuhani.
- njaa
-
ukosefu wa chakula kwa sababu hakuna cha kutosha kulisha kila mtu
- nyika
-
mahali ambapo hakuna miji ama vijiji na watu wachache wanaishi hapo
- nyumba ya wageni
-
mahali ambapo watu wanaweza kula na kulala wakati wakiwa safarini
- nzige
-
mdudu mkubwa anayeruka wakati mwingine hutumika kama chakula
Pichanzige - okoa
-
kukomboa kutoka kwenye hatari. Yesu alikufa ili kutuokoa kutokana na kifo cha kimwili na hatari za dhambi.
- ongoza
-
kuwaongoza wengine
- ono
-
aina ya ufunuo kutoka kwa Baba wa Mbinguni
- pango
-
shimo katika upande wa mlima
Pichapango - Pasaka
-
sherehe maalumu ambapo Wayahudi hukumbuka jinsi Mungu alivyowaokoa watu wao kutoka kwa Wamisri wakati wa Musa
- piga magoti [kupiga magoti]
-
kwenda chini kwa magoti yako
PichaKupiga magoti - ponya
-
kufanya mtu aliye mgonjwa ama aliye umia kuwa mzima
- roho
-
mmoja wa watoto wa Baba wa Mbinguni ambaye hana mwili wa nyama na mifupa
- Sabato
-
siku maalumu ya wiki ambapo watu humwabudu Mungu kwa kwenda kanisani na kujifunza zaidi kuhusu Yeye
- safiri
-
kwenda kutoka sehemu moja hadi nyingine
- sakramenti
-
ibada ambapo mkate na maji hubarikiwa na kupewa waumini wa Kanisa ili kuwakumbusha juu ya Yesu Kristo na kutii amri. Ibada hiyo hufanywa na wanaume ambao wana ukuhani.
- sala
-
yale yanayosemwa wakati mtu anaposali
- sali
-
kuzungumza na Mungu, ukimpa shukrani na kuomba baraka
- saliti
-
kumgeuka rafiki au kumkabithi kwa adui
- samehe
-
kuacha kumkasirikia mtu ambaye amefanya vitu vibaya au vya kudhuru
- sarafu
-
kipande cha pesa, kilicho bapa
Pichasarafu - sega la asali
-
vyumba vya nta vilivyotengenezwa na nyuki. Nyuki hujaza vyumba hivi vya nta kwa asali.
Pichasega la asali - sherehekea
-
kukumbuka siku muhimu kwa kufanya kitu maalumu
- shitaka
-
tukio ambapo watu hujaribu kuthibitisha ikiwa mtu amevunja sheria au la
- shuhudia
-
kuwaambia watu wengine kwamba tunajua kitu fulani ni cha kweli
- sifu
-
kusema mambo mazuri kuhusu mtu fulani
- sinagogi
-
jengo ambapo Wayahudi hukutana ili kumwabudu Mungu
- sulubisha
-
kuua mtu kwa kumning’iniza kwenye msalaba wa mbao kama walivyomfanyia Yesu Kristo
- tafsiri
-
kubadilisha maneno yaliyoandikwa ama kuzungumzwa katika lugha moja kwenye maneno yaliyo na maana sawa katika lugha tofauti
- taji ya miiba
-
miiba mikali iliyopangwa kwa duara iliyowekwa kichwani kwa Yesu
Pichataji ya miiba - takatifu
-
kitu ambacho ni halisi na kisafi na kilichotengwa kwa ajili ya matumizi ya Mungu
- takatifu
-
chochote kilichotolewa kwetu na Mungu ambacho ni cha kuheshimiwa na kustahiwa
- tawaza
-
wanaume ambao wana ukuhani wanaweka mikono yao juu ya kichwa cha mwanaume mwingine ili kumpa nguvu na mamlaka ya ukuhani
Pichautawazo - teka [tekwa]
-
kuchukua nchi ama mtu kwa nguvu
- teseka
-
kuhisi uchungu mwingi
- tetemeko la ardhi
-
mtetemo wa nguvu sana wa ardhi
- tii
-
kufanya kile ambacho kinatakiwa au kuamriwa
- tubu
-
kuhisi huzuni kwa jambo ulilofanya na kuahidi kamwe kutolirudia tena
- ubatizo [batiza]
-
ibada ama utaratibu ambapo mtu mwenye mamlaka ya ukuhani kutoka kwa Mungu anamweka mtu mwingine ndani kabisa ya maji na kumwinua kutoka kwenye maji. Ubatizo unahitajika ili kuwa muumini wa Kanisa la Yesu Kristo. Pia ona Kipawa cha Roho Mtakatifu.
Pichaubatizo - ufalme wa Mungu
-
Kanisa ama mahali ambapo waadilifu wataishi na Baba wa Mbinguni baada ya maisha haya
- ufunuo
-
kitu Mungu huwaambia watu Wake
- Ujio wa Pili
-
wakati Yesu atakaporudi duniani tena ili kuokoa watu waadilifu na kuwaangamiza waovu
- ukuhani
-
mamlaka ya kutenda katika jina la Mungu
- ukweli
-
kile ambacho ni cha kweli na sahihi
- uovu
-
kitu ambacho ni kibaya na hakitoki kwa Mungu
- ushuhuda
-
hisia ama wazo kutoka kwa Roho Mtakatifu kwamba injili ni ya kweli
- ushuru
-
pesa ambazo watu hulipa serikalini
- uzima wa milele
-
kuwa kama Baba wa Mbinguni na kuishi Naye milele
- vita
-
mapigano kati ya maadui
- wimbo
-
wimbo wa kanisa ama wimbo unaomtukuza Mungu
- wokovu
-
kuokolewa kutokana na dhambi na kifo ili tuweze kuishi na Baba wa Mbinguni tena
- zaa
-
kutengeneza ama kukuza kitu
- zaka
-
pesa ambayo hutolewa kwa Mungu ili kujenga Kanisa Lake
- zama
-
kufa kwa kuwa majini kwa muda mrefu sana
- zawadi
-
kitu kizuri ambacho Mungu ama wengine hutupatia
- zika [zikwa]
-
kuweka mwili wa mtu aliyekufa katika kaburi au ardhini na kufunika kwa udongo; kuweka kitu fulani ardhini ambacho mtu anataka kuficha