Sura ya 60
Petro Anamfufua Tabitha
Picha
mwanamke akisaidia watu
Mwanamke mwema aliyeitwa Tabitha aliishi katika mji wa Yafa. Alikuwa mfuasi wa Yesu Kristo. Aliwasaidia watu wengi na kufanya mambo mengi mema.
Picha
watu wakilia pembeni mwa kitanda cha mwanamke
Alikuwa mgonjwa na akafa.
Picha
Petro pembeni mwa kitanda cha mwanamke
Rafiki zake walimwita Petro. Alipofika pale, aliwaomba rafiki za Tabitha waondoke chumbani.
Picha
Petro akimsaidia mwanamke kukaa vizuri
Petro alipiga magoti na kuomba, kisha akamwambia Tabitha asimame. Alifungua macho yake na alikaa vizuri.
Picha
Petro akimsaidia mwanamke kutembea
Petro alimsaidia kusimama. Aliwaita rafiki zake. Walikuja na kuona kwamba alikuwa hai. Petro alikuwa ametumia nguvu ya ukuhani kumfufua Tabitha. Watu wengi huko Yafa waliamini katika Yesu Kristo pale walipogundua juu ya ufufuo wa Tabitha.