Sura ya 51
Yesu Anateseka katika Bustani ya Gethsemane
Yesu na Mitume walienda kwenye Bustani ya Gethsemane. Yuda hakwenda pamoja nao. Alienda kuwaambia viongozi wa Kiyahudi mahali Yesu alipokuwa.
Yesu aliwaomba Petro, Yakobo na Yohana kwenda pamoja Naye katika bustani. Aliwasihi wamngoje wakati alipokwenda kuomba.
Yesu alijua alihitaji kuteseka kwa ajili ya dhambi za watu wote. Hakutaka kuteseka, lakini alichagua kumtii Baba wa Mbinguni.
Petro, Yakobo, na Yohana walilala wakati Yesu akiomba. Yesu alikuja na kuwakuta wamelala. Aliwaambia wawe macho.
Alienda kuomba tena. Petro, Yakobo na Yohana walitaka kubaki macho, lakini walikuwa wamechoka sana. Walilala tena. Yesu aliwakuta wamelala tena. Alienda na kuomba kwa mara ya tatu.
Yesu alipokuwa akisali, Alianza kutetemeka kwa sababu ya uchungu. Malaika alikuja kumpa nguvu. Aliteseka sana kiasi kwamba alitokwa na jasho la matone ya damu. Alikuwa akiteseka kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba tuweze kusamehewa tukitubu.
Yesu aliwaamsha Petro, Yakobo na Yohana. Aliwaambia kwamba angesalitiwa na kuuwawa. Yesu alisema kwamba watu waovu walikuwa wanakuja kumchukua.