Scripture Stories
Sura ya 18: Yesu Anachagua Mitume Wake


Sura ya 18

Yesu Anachagua Mitume Wake

Picha
Yesu ndani ya mashua

Siku moja Yesu aliwafundisha watu kutoka kwenye mashua kwenye ufukwe wa Bahari ya Galilaya. Mashua ilikuwa ni ya Mtu aliyeitwa Petro.

Picha
Yesu ndani ya mashua

Petro na rafiki zake walikuwa wamevua samaki usiku mzima bila ya kushika samaki wowote. Baada ya Yesu kumaliza kufundisha, Alimwambia Petro apeleke mashua kilindini. Kisha akamwambia Petro na rafiki zake washushe nyavu zao za kuvua majini.

Picha
wavuvi wakivua samaki

Walivua samaki wengi sana hadi nyavu zao zikaanza kukatika.

Picha
wavuvi ndani ya mashua

Petro aliwaita rafiki zake katika mashua nyingine kuja kuwasaidia. Samaki walijaza mashua zote mbili kiasi kwamba zikaanza kuzama.

Picha
wavuvi ndani ya mashua

Petro na rafiki zake walishangaa. Walijua kwamba Yesu Kristo alikuwa amefanya hili litendeke.

Picha
Petro akiwa amepiga magoti mbele ya Yesu

Petro alipiga magoti kwenye miguu ya Mwokozi. Alisema kwamba hakustahili kuwa karibu na Yesu. Yesu alimwambia Petro asiwe na hofu.

Picha
Yesu akiwafundisha wavuvi

Marafiki wawili wa Petro, Yakobo na Yohana, walikuwa ndugu. Yesu aliwaambia Petro, Yakobo na Yohana wamfuate na wawe “wavuvi wa watu.” Wanaume hao waliacha kila kitu walichokuwa nacho na kwenda pamoja na Yesu. Mwokozi pia aliwaambia wanaume wengine wamfuate Yeye.

Picha
Yesu na Mitume 12

Yesu aliwachagua Mitume kumi na wawili waongoze Kanisa Lake. Aliomba usiku mzima ili kwamba angeweza kuchagua wanaume wanaofaa. Asubuhi iliyofuata alichagua na kuwatawaza wanaume kumi na wawili, akiwapa ukuhani na mamlaka ya kuwa Mitume.

Picha
Mitume wakisafiri

Mitume walisafiri kwenda miji mingi. Walifundisha injili na kuwaponya watu. Walirudi kumwambia Yesu kile walichokuwa wamefanya.

Chapisha