Sura ya 24
Binti wa Yairo Anafufuliwa kutoka Wafu
Siku moja Yairo, mtawala wa sinagogi, alianguka miguuni pa Mwokozi.
Yairo alisema kwamba binti yake wa miaka 12 alikuwa mgonjwa sana. Alimuomba Yesu aende na kumbariki. Aliamini kwamba Yesu angemponya.
Yesu alianza kumfuata Yairo nyumbani, lakini alisimama ili kumponya mwanamke. Alipokuwa akiongea naye, mtu alikuja kumwambia Yairo kwamba alikuwa amechelewa sana—bintiye alikuwa amekufa.
Yesu alisikia kile kilichosemwa. Alimwambia Yairo asiwe na hofu lakini amuamini Yeye.
Kisha Yesu akaenda na Yairo nyumbani kwake. Nyumba ilikuwa imejaa watu ambao walikuwa wakilia kwa sababu ya kifo cha msichana huyo mdogo.
Yesu aliwaambia kwamba msichana hakuwa amekufa ila alikuwa amelala. Watu walimcheka. Walikuwa na uhakika msichana alikuwa amekufa.
Mwokozi alitaka kila mtu aondoke ndani ya nyumba isipokuwa wanafunzi Wake, Yairo na mkewe Yairo. Walienda chumbani ambako msichana huyo mdogo alikuwa amelala.
Yesu alimshika msichana kwa mkono. Alimwambia aamke. Alisimama na kutembea. Wazazi wake walishangaa. Yesu aliwaambia wasimwambie yeyote kile kilichotokea. Kisha Yeye aliwaambia wazazi wake wampe msichana kitu cha kula.