Agano la Kale 2022
Mei 16–22. Kumbukumbu la Torati 6–8; 15; 18; 29–30; 34: “Ujitunze, Usije Ukamsahau Bwana”


“Mei 16–22. Kumbukumbu ya Torati 6–8; 15; 18; 29–30; 34: ‘Ujitunze, Usije Ukamsahau Bwana’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Mei 16–22. Kumbukumbu la Torati 6–8; 15; 18; 29–30; 34,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Musa amesimama juu ya mlima

Kielelezo cha Musa juu ya Mlima Nebo, © Providence Collection/licensed from goodsalt.com

Mei 16–22

Kumbukumbu la Torati 6–8; 15; 18; 29–30; 34

“Ujitunze, Usije Ukamsahau Bwana”

Tafakari jinsi unavyoweza kutohoa shughuli katika muhtasari huu kwa mahitaji ya watoto unaowafundisha. Kwa mfano, kama unafundisha watoto wadogo, unaweza kuwasaidia wao kujiandaa kwa ajili ya ubatizo kwa kutohoa shughuli zipatikanazo kwenye “Kutunza maagano yangu huleta baraka kuu” katika sehemu ya watoto wakubwa.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto washiriki mambo waliyojifunza kuhusu Musa katika Msingi au nyumbani katika wiki chache zilizopita. Kama itahitajika, onyesha picha za matukio kutoka katika maisha ya Musa ili kuwasaidia kukumbuka. Waambie kwamba leo utazungumza kuhusu mambo ambayo Musa alifundisha mwishoni mwa maisha yake ya duniani.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Kumbukumbu ya Torati 6:5

Ninaweza kumpenda Bwana kwa moyo wangu wote.

Musa aliwafundisha wana wa Israeli kwamba wanapaswa kumpenda Bwana kwa moyo wao wote, roho, na nguvu zao zote. Fikiria juu ya njia unazoweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kuzidisha upendo wao kwa Baba wa Mbinguni na Mwokozi.

Shughuli Yamkini

  • Chora moyo ubaoni, umbo la mwili, na mkono wenye nguvu. Soma Kumbukumbu la Torati 6:5, na uoneshe kwa kidole picha unaposoma maneno “moyo” “nafsi” na “nguvu.” Waalike watoto kuchukua zamu kuonyesha kwa kidole picha wakati darasa linarudia kifungu cha maandiko pamoja nawe.

  • Imba wimbo ambao unafundisha kuhusu upendo wa Mungu, kama vile “My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 228–29). Wasaidie watoto kutafuta maneno katika wimbo ambayo yanaonyesha kwamba Baba wa Mbinguni anatupenda. Wasaidie kufikiria juu ya njia tunazoweza kumwonyesha kwamba sisi pia tunampenda Yeye.

Kumbukumbu la Torati 6:6–9

Maandiko ni neno la Mungu

Ushauri katika Kumbukumbu la Torati 6:6–9 ulikusudiwa kuwasaidia Waisraeli “Wajitunze wasije wakamsahau Bwana” na neno Lake (mstari wa 12). Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto kufanya maandiko kuwa sehemu thabiti ya maisha yao?

Shughuli Yamkini

  • Mwalike mtoto afiche nakala ya maandiko ndani ya chumba wakati watoto wengine wakifumba macho yao. Kisha waambie watoto wafumbue macho yao, wajaribu kutafuta maandiko. Ukitumia vifungu vya maneno muhimu kutoka kwenye Kumbukumbu la Torati 6:6–9, shiriki na watoto kwamba Musa aliwambia Waisraeli waweke vifungu vya maneno katika sehemu ambazo wataviona na kujifunza kutoka kwayo kila siku. Wasaidie watoto kufikiria juu ya sehemu katika nyumba zao ambapo wanaweza kuyaweka maandiko ili waweze kuyaona kila siku.

  • Imba wimbo kuhusu maandiko, kama vile “Search, Ponder, and Pray” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,109). Shiriki ushuhuda wako kwamba maandiko ni neno la Mungu, na uwaambie watoto jinsi yanavyobariki maisha yako.

Picha
Yesu amepiga goti huku akimshikilia mtu

Yesu Kristo ni nabii kama vile Musa.

Kumbukumbu la Torati 18:15–18

Manabii hutufundisha kuhusu Yesu Kristo.

Musa alitoa unabii kwamba Yesu Kristo angekuja, na kwamba tunapaswa kusikiliza maneno ambayo Yesu angefundisha.

Shughuli Yamkini

  • Msaidie mmojawapo wa watoto kusoma Kumbukumbu la Torati 18:18, na uwaambie watoto kwamba Nabii kama Musa ambaye Mungu angemuinua ni Yesu Kristo. Ili kuwasaidia watoto kuona njia ambazo kwazo Musa na Yesu wanalingana, lete picha za mambo ambayo Musa alitenda na mambo ambayo Yesu Kristo alitenda, na waache watoto waoanishe. Kwa mfano, unaweza kuleta picha za Musa na Yesu wakiwatawaza na kuwafundisha wengine (ona Kitabu cha Sanaa ya injili, na. 15, 16, 3839).

  • Waoneshe watoto picha ya nabii wetu wa sasa, na shiriki kitu fulani ambacho amefundisha kuhusu Mwokozi. Alika watoto kuchora picha ya nabii ili kushiriki na familia zao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Kumbukumbu la Torati 6:6–9

Ninaweza kuliweka neno la Mungu katika moyo wangu.

Musa alifundisha kwamba tunapaswa kuliweka neno la Mungu katika mioyo yetu, na aliwapa Waisraeli ushauri kuhusu jinsi ya kuweka neno la Mungu daima mbele zao. Ni kwa jinsi gani utawatia moyo watoto kujifunza kutoka kwenye neno la Mungu kila siku.

Shughuli Yamkini

  • Ubaoni, andika maneno na vifungu vya maneno kutoka Kumbukumbu la Torati 6:6–9 ambavyo vinaashiria ni wakati gani na namna gani Waisraeli walipaswa kukumbuka neno la Mungu (kama vile uketipo, utembeapo, ulalapo, mkono, na nyumba). Waalike watoto kutafuta maneno haya katika mistari. Ni nini maneno haya hutufundisha kuhusu jinsi ya kufanya maandiko kuwa sehemu yetu ya maisha ya kila siku? Waulize watoto kile wanachoweza kufanya kukumbuka neno la Mungu katika maisha yao ya kila siku.

  • Mpatie kila mtoto kipande cha karatasi, na waalike waandike kifungu cha maneno kutoka katika Kumbukumbu la Torati 6 ambacho ni muhimu kwao. Waombe washiriki kwa nini walichagua kifungu chao cha maneno. Pendekeza kwamba wapambe karatasi zao na kuzitundika nyumbani kwao ili wayakumbuke. Wahimize watoto waandike na kutundika vifungu vingine wanavyovipata katika maandiko.

Kumbukumbu la Torati 15:7–11

Ninaweza kuwahudumia kwa furaha wale walio na mahitaji.

Mafundisho katika Kumbukumbu la Torati 15:7–11 yanaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kuelewa kwamba kuwasaidia wengine kunahusisha zaidi ya vitendo tu. Inapaswa kufanywa kwa moyo mkujufu.

Shughuli Yamkini

  • Andika nani, kwa nini, na kwa jinsi gani ubaoni. Waalike watoto wasome Kumbukumbu la Torati 15:7–11 ili kujua ni nani tunapaswa kumsaidia, kwa nini tunapaswa kuwasaidia wao, na ni kwa jinsi gani mioyo yetu inapaswa kuhisi kuhusu kusaidia. Waache waandike ubaoni kile wanachopata. Imbeni wimbo ambao unaimarisha ujumbe katika mistari hii, kama vile “Have I Done Any Good?” (Nyimbo, na. 223).

  • Waombe watoto kumfikiria mtu wanayeweza kumsaidia—hususani katika familia zao wenyewe. Wape muda kwa ajili yao kuandika kile watakachofanya wiki hii kumsaidia mtu huyo. Kama inawezekana, fanyeni mipango kama darasa ya kumfikia mtu fulani mwenye mahitaji.

Kumbukumbu la Torati 30:8–10

Kuweka maagano yangu huleta baraka kuu.

Kama wana wa Israeli, sisi tunahitaji kukumbushwa daima kuishi maagano yetu. Kusoma Kumbukumbu la Torati 30:8–10 kunaweza kuwasaidia watoto kuelewa vyema maagano ni nini na watie moyo kushika maagano yao.

Shughuli Yamkini

  • Waulize watoto maagano ni nini (kama wanahitaji msaada, pendekeza kwamba watafute maelezo katika “Agano” katika Mwongozo wa Maandiko [scriptures.ChurchofJesusChrist.org]). Chora jedwali lenye safu mbili ubaoni lenye vichwa Ahadi za Waisraeli na Ahadi za Mungu. Waalike watoto wapekue Kumbukumbu la Torati 30:8–10 na wajaze jedwali. (Kama lazima, wasaidie watoto kuelewa maana ya vifungu vya maneno katika mstari wa 9.) Shuhudia juu ya baraka ambazo zimekuja kwako kutokana na kuishi maagano yako.

  • Waalike watoto waorodheshe kwenye ubao ahadi tunazofanya wakati wa ubatizo na ahadi Baba wa Mbinguni huzifanya kwetu (ona Mafundisho na Maagano 20:37, 77). Tunaweza kufanya nini ili daima tumkumbuke Mwokozi na kushika maagano yetu?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto wajifanye kuwa wewe ni mwanafamilia yao, na uwaulize wakuambie kitu kimoja walichojifunza leo darasani. Wahimize washiriki kile walichokuambia pamoja na mmoja wa wanafamilia wao wakati watakapofika nyumbani.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Uliza maswali yenye uvuvio. Uliza maswali yanayoalika watoto sio tu kutoa ripoti ya mambo bali kushiriki shuhuda zao za kweli za injili. Kwa mfano, kama unajadili amri, unaweza kuwaomba watoto kushiriki ni kwa jinsi gani kutii amri kumewabariki.

Chapisha