Agano la Kale 2022
Julai 11–17. 2 Wafalme 17–25: “Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli”


Julai 11–17. 2 Wafalme 17–25: ‘Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israel’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Julai 11–17. 2 Wafalme 17–25,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
watu wanaondoka kutoka jiji lililoangamizwa

Kutoroka kwa Wafungwa, na James Tissot and others

Julai 11–17

2 Wafalme 17–25

“Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli”

Unapopanga shughuli za kujifunza kwa ajili ya watoto, kumbuka kwamba shughuli kwa ajili ya watoto wadogo katika muhtasari huu zinaweza kutoholewa kwa ajili ya watoto wakubwa, na kinyume chake.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Andika jina la kila mtoto katika kipande cha karatasi, na uweke vipande hivyo ndani ya chombo. Mwanzoni mwa darasa, waache watoto waje kwa zamu kuchagua jina. Wakati jina la mtoto limetwaliwa, mtake mtoto yule ashiriki jambo alilojifunza kuhusu injili au kumhusu Yesu Kristo hivi karibuni. Endelea hivi mpaka kila mtoto awe amepata nafasi ya kushiriki.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

2 Wafalme 18:3, 5

Ninaweza kumtumainia Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Mfano wa Hezekia katika 2 Wafalme 18:3, 5 unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kuweka matumaini yao kwa Mungu.

Shughuli Yamkini

  • Taja vitu vichache ambavyo mfalme mzuri angeweza kufanya na vitu fulani mfalme mbaya angeweza kufanya. Waombe watoto wasimame na kushangilia kwa vitu vizuri na kukaa chini kwa vitu vibaya. Waeleze watoto kwamba Israeli ilikuwa na wafalme wengi, baadhi yao walikuwa wema na wengine hawakuwa wema. Waalike watoto wasikilize kile kilichomfanya Hezekia kuwa mfalme mzuri unaposoma 2 Wafalme 18:3, 5. Wasaidie kufikiria juu ya njia tunazoweza kuonyesha kwamba tunamtumainia Bwana kama Hezekia alivyofanya.

  • Wasaidie watoto kuelewa inamaanisha nini kumtumaini mtu. Zungumzia kuhusu watu unaowatumaini, na waache watoto wafanye vivyo hivyo. Onyesha picha ya Yesu Kristo. Kwa nini tunaweza kumtumaini Yesu Kristo? Onyesha matumaini yako kwamba Yesu Kristo anatupenda na atatusaida kurudi kuishi milele na Baba wa Mbinguni.

2 Wafalme 22:8–11; 23:2

Maandiko ni baraka.

Hata ingawa watoto wadogo hawawezi kusoma au kuelewa kila kitu katika maandiko, wanaweza kubarikiwa na nguvu za maandiko. Unaweza kufanya nini kuwasaidia kuwa na shauku ya kubarikiwa na neno la Mungu?

Shughuli Yamkini

  • Ficha nakala ya maandiko mahali fulani chumbani, na watake watoto kuitafuta. Elezea kwamba katika siku za Mfalme Yosia, watu wengi hawakuwa wakijifunza kutoka kwenye maandiko mpaka kuhani alipoyapata katika hekalu (ona 2 Wafalme 22:8–11. Je, ni maandiko yapi? Kwa nini tunahitaji maandiko? Waambie watoto kwa nini una furaha kwamba tuna maandiko leo, na uwaache washiriki hisia zao kuhusu maandiko.

  • Wasomee watoto 2 Wafalme 23:2 na waombe wasikilize kile ambacho mfalme alifanya na maandiko. Je, kwa nini ni muhimu kwa kila mtu kusikia kile kilichoandikwa katika maandiko? Imbeni wimbo kuhusu maandiko, kama vile “Search, Ponder, and Pray,” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 109), na waombe watoto wazungumze kuhusu jinsi wanavyohisi wanaposikia mafundisho na hadithi kutoka kwenye maandiko.

    Picha
    familia ikijifunza maandiko

    Maandiko yanaweza kutatusaidia kuigeuza mioyo yetu kwa Bwana.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

2 Wafalme 18:3–6; 19:14–19

Ninaweza kuwatumainia Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Wakati Waashuri walitishia Yerusalemu, Hezekia Mfalme mwema alimgeukia Bwana kwa imani. Mfano wa Hezekia unaweza kukusaidia wewe na watoto kuzungumza kuhusu jinsi tunavyoweza kuonyesha imani yetu katika Bwana, hata wakati imani hiyo inapata changamoto.

Shughuli Yamkini

  • Ukitumia ramani na. 3 ya Biblia, “The Division of the 12 Tribes,” kwa kifupi waelezee watoto kwamba Ufalme wa Israeli wa Kaskazini ulitekwa na watu walioitwa Waashuri. Elezea kwamba Waashuri baadaye walijaribu kuteka Ufalme wa Yuda wa Kusini. Waalike watoto wafikirie jinsi ambavyo wangehisi kama wangekuwa wanaishi katika Yuda na walijua kwamba Waashuri walikuwa wanakuja kuangamiza mji huo. Waombe watoto wasome 2 Wafalme 18:3, 5–6 ili kujua kwa nini Hezekia, mfalme wa Yuda, aliweza kuwa jasiri wakati Waashuri walipokuja.

  • Waalike watoto wasome 2 Wafalme 19:14–19, wakitafuta kile Hezekia alifanya wakati Waashuri walitishia ufalme wake. Ni kwa jinsi gani kufanya mambo haya kulionyesha kwamba alimtumaini Bwana? Nini tunaweza kufanya kuonesha matuamini yetu kwa Mwokozi wakati tunapohitaji msaada?

2 Wafalme 22:8–13; 23:2–3

Maandiko yananifundisha jinsi ya kumfuata Yesu Kristo.

Baada ya miaka ya giza la kiroho, Wayahudi walifanya upya dhamira yao ya kumfuata Bwana. Hili lilitokea kwa sababu Mfalme Yosia aligundua upya kitabu cha torati na kuwasomea watu. Tukio hili linaweza kuwasaidia watoto kuelewa kwa nini maandiko ni ya thamani sana.

Shughuli Yamkini

  • Waambie watoto kwamba Mfalme Yosia aliwaambia watu wake wakarabati hekalu, na walipofanya hivyo, walipata kitu cha thamani sana. Waalike watoto wasome 2 Wafalme 22:8–11 ili kujua kilikuwa kitu gani. Elezea kwamba kitabu walichokipata kilikuwa na maagano na amri ambazo wana wa Israeli hawakujua kuzihusu. Ni nini kingetokea kwetu kama hatungekuwa na maandiko? Waulize watoto kwa nini wana shukrani kwa kuwa na maandiko? Kwa nini ingekuwa vigumu sana kumfuata Mwokozi kama hatungekuwa na maandiko?

  • Mpe kila mtoto kipande cha karatasi, na uwaombe wakichane. Elezea kwamba katika siku za Mfalme Yosia, watu wakati fulani walichana, au “kurarua,” nguo zao wakati wamekasirika. Waombe watoto watafute neno “akararua” katika 2 Wafalme 22:11. Ni nini kingemfanya Yosia kukasirika? Waalike watoto kupata jibu katika mstari wa 13. Kwa nini ni muhimu kwetu kusoma maandiko kila mara?

  • Someni 2 Wafalme 23:2–3 kwa pamoja, na waombe watoto watafute jinsi maandiko yalivyomsaidia Yosia na watu wake. Shiriki pamoja na watoto andiko ambalo limekutia moyo “kumfuata Bwana” (mstari wa 3), na uwaalike watoto kushiriki maandiko ambayo yamewasaidia. Imbeni pamoja “I Will Walk with Jesus” (ChurchofJesusChrist.org).

2 Wafalme 23:3

Nitayashika maagano yangu na Mungu.

Wakati Yosia na watu wake walipojifunza amri za Mungu, walifanya agano la kuziishi. Unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha wawe na shauku ya kubaki waaminifu kwa maagano waliyofanya katika ubatizo.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wasome 2 Wafalme 23:3 na watafute maneno na vifungu vya maneno ambavyo vinaonyesha jinsi watu walivyohisi kuhusu amri za Bwana. Waalike wasimame na kuzungumza kuhusu nini ingemaanisha “[kusimama] kwenye maagano.” Waalike watembee papohapo walipo na kuzungumzia kuhusu “kumfuata Bwana” kunamaanisha nini. Waalike waweke mikono yao kwenye mioyo yao na kupendekeza njia wanazoweza kutii amri “kwa mioyo yao yote.”

  • Wasaidie watoto kutengeneza orodha ya ahadi tulizofanya wakati wa ubatizo (ona Mosia 18:10; Mafundisho na Maagano 20:37, 77, 79). Mungu anatuahidi nini kama tutashika maagano yetu? Tunajifunza nini kutoka 2 Wafalme 23:3 kuhusu jinsi tunavyopaswa kushika maagano yetu?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto washiriki pamoja na mwanafamilia mstari wa maandiko au hadithi kutoka kwenye maandiko ambayo iliwabariki.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kuwajengea watoto kujiamini. Njia moja ya kuwasaidia watoto kujenga kujiamini ni kuwasifia wanaposhiriki katika darasa. Waahidi watoto kwamba Roho Mtakatifu atawasaidia wanapojifunza.

Chapisha