Agano la Kale 2022
Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7: “Yuko Nabii katika Israeli”


“Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7: ‘Yuko Nabii katika Israeli’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Elisha akimwonyesha mtumishi magari ya moto

Kielelezo cha Elisha akimwonyesha mtumishi magari ya moto, © Review & Herald Publishing/licensed from goodsalt.com

Julai 4–10

2 Wafalme 2–7

“Yuko Nabii katika Israeli”

Shughuli katika muhtasari huu zimekusudiwa kuamsha mawazo yako mwenyewe ya ubunifu. Kupitia kujifunza kwa maombi, unaweza kupokea mwongozo wa kukidhi mahitaji ya watoto unaowafundisha.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wahimize watoto kushiriki kile wanachojua kuhusu nabii Elisha, waalike wao wachore picha ya kitu alichofanya.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

2 Wafalme 4–5

Mungu anaweza kufanya miujiza katika maisha yangu.

Kupitia nabii Elisha, Bwana aliwabariki watu wengi katika njia za kustaajabisha. Wasaidie watoto kutambua miujiza ya Bwana katika maisha yao.

Shughuli Yamkini

  • Shiriki muujiza mmoja au mingi ilioandikwa katika 2 Wafalme 4–5 (ona “Elisha Nabii” na “Elisha Anamponya Naamani” katika Hadithi za Agano la Kale). Waache watoto washiriki kile wanachopenda kuhusu na hadithi hizi. Waalike wasimulianae tena hadithi hizi wao kwa wao.

  • Shuhudia kwamba Bwana anaweza kutumia nguvu Zake kufanya vitu vikubwa kutusaidia. Tunaita vitu hivi miujiza. Shiriki jinsi Bwana alivyoonyesha upendo Wake kwako katika njia ambazo ni kubwa au ndogo. Imbeni pamoja wimbo kuhusu upendo wa Mungu, kama vile “My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 228–29). Waombe watoto washiriki jinsi wanavyojua kwamba Mungu anawapenda.

2 Wafalme 5:1–15

Ninaweza kuchagua kufanya kile Mungu anachoamuru kupitia nabii Wake.

Naamani alikuwa na wakati mgumu kutii wakati nabii Elisha alipomwambia jinsi ya kuponywa ukoma. Tafakari jinsi unavyoweza kuwasaidia watoto kuelewa baraka ambazo huja kwa kuwa watiifu.

Shughuli Yamkini

  • Simulia hadithi ya Naamani (ona 2 Wafalme 5:9–14; “Elisha Anamponya Naamani” katika Hadithi za Agano la Kale; ona pia picha ya Naamani katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia). Sisitiza kwamba hapo mwanzo Naamani hakutaka kuoga katika Mto Yordani, hata ingawa Elisha alimwambia kwamba hii ingemponya ugonjwa wake. Simulia wakati ambapo hukuwa na uhakika kama ulihitaji kufanya kitu kilicho sahihi, na kuwasaidia watoto kufikiria mifano yao wenyewe. Kisha shiriki jinsi Naamani alivyobarikiwa alipofanya uamuzi sahihi.

  • Wasomee watoto 2 Wafalme 5:13 na uelezee kwamba mtumishi wa Naamani alimsaidia kufanya uamuzi wa kumtii nabii Elisha. Wasaidie watoto kufikiria njia wanazoweza kuwasaidia rafiki zao au wanafamilia wao kumsikilza na kumtii nabii.

2 Wafalme 6:8–17

Bwana ananilinda mimi.

Wakati mtumishi wa Elisha alipoona jeshi la Shamu limewazunguka, aliogopa sana. Hata hivyo, Elisha alimwambia “usiogope” kwa sababu Bwana alikuwa pamoja nao (2 Wafalme 6:16).

Shughuli Yamkini

  • Wasomee watoto 2 Wafalme 6:15 au fafanua ili waweze kuelewa. Waalike watoto kufikiria kwamba wamezingirwa na jeshi kubwa lenye farasi na magari, kama vile mtumishi wa Elisha. Wangehisi vipi? Wangefanya nini? Waombe wafumbe macho wakati unasoma 2 Wafalme 6:16–7. Wakati unapofika kwenye maneno “fumbua macho yake,” waombe watoto wafumbue macho yao. Waelezee kile ambacho mtumishi aliona kikimlinda yeye na Elisha. Shiriki jinsi unavyojua Bwana anatulinda.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu ulinzi wa Mungu kwetu, kama vile ubeti wa mwisho wa “Dearest Children, God Is Near You” (Nyimbo za Watoto, na. 96). Badilisha maneno katika wimbo na majina ya watoto kusisitiza kwamba Mungu anawalinda.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

2 Wafalme 4–5

Mungu anaweza kufanya miujiza katika maisha yangu.

Wakati wa huduma yake, Elisha aliponya na kubariki watu wengi. Ni kwa jinsi gani miujiza katika 2 Wafalme 4–5 inawasaidia watoto kutambua mkono wa Baba wa Mbinguni katika maisha yao?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kuandika ubaoni miujiza mingi wanayoweza kukumbuka kutoka katika maandiko. Kisha wape muda kupitia upya 2 Wafalme 4–5 na waongeze katika orodha yao (ona 2 Wafalme 4:1–7, 14–17, 32–35, 38–41, 42–44; 5:10–14). Je, miujiza hii inafundisha nini kuhusu jinsi Baba wa Mbinguni anavyohisi kutuhusu sisi?

  • Waombe watoto kuzungumza kuhusu muujiza ni nini. Kama wanahitaji msaada, wangeweza kupitia upya “Muujiza” katika Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org). Waalike kushiriki baadhi ya miujiza ambayo Yesu alifanya. Zungumza kuhusu jinsi ulivyoona nguvu za Mungu katika maisha yako. Unaweza kujumuisha miujiza ya kila siku kama vile hisia za amani, zawadi ya maisha ya kila siku, au msaada katika kazi za kila siku. Waalike watoto wazungumze kuhusu miujiza katika maisha yao, yote mikubwa na midogo.

2 Wafalme 5:1–15

Ninaweza kuchagua kuwa mwaminifu, mnyenyekevu na mtiifu.

Naamani alitaka kuponywa ukoma, lakini hakutarajia maelekezo rahisi ambayo Elisha alimpa: “Enenda ukaoge katika Yordani mara saba” (2 Wafalme 5:10). Fikiria jinsi unavyoweza kutumia hadithi hii kuwafundisha watoto kuhusu imani katika Yesu Kristo, unyenyekevu, na utiifu.

Shughuli Yamkini

  • Andika imani, unyenyekevu na utiifu ubaoni, na waulize watoto kile maneno haya yanamaanisha (ona Kweli kwa Imani, 54–56, 88–87, 108–9). Waalike watoto wasome Wafalme 5:9–14. Ungeweza pia kuonesha sehemu za video “Naamani na Elisha” (ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa jinsi gani Naamani alionyesha imani yake katika Bwana, unyenyekevu, na utiifu? Kwa nini ni muhimu kwetu kuwa na sifa hizi?

  • Waombe watoto waeleze kuhusu wakati ambapo rafiki aliwasaidia kuchagua kile kilicho sahihi. Pia shiriki uzoefu wako mwenyewe. Someni pamoja 2 Wafalme 5:10–13 ili kujifunza jinsi mtumishi wa Naamani alivyomsaidia kuchagua kumtii nabii. Tunaweza kufanya nini kusaidiana kumfuata nabii wetu leo?

  • Waalike watoto wakamilishe ukurasa wa shughuli na kushiriki na mwanafamilia au rafiki nini walichojifunza kutoka kwa hadithi ya Naamani katika 2 Wafalme 5:1–15.

2 Wafalme 6:8–17

Mimi siko peke yangu.

Watoto unaowafundisha wakati mwingine wanaweza kuhisi kama mtumishi wa Elisha—kukosa uhakika wa jinsi ya kukabiliana na changamoto zilizopo mbele yao. Unaweza kutumia tukio katika 2 Wafalme 6:8–17 kuwafundisha wao “kutoogopa” kwa sababu Bwana hajawaacha peke yao.

Shughuli Yamkini

  • Someni pamoja 2 Wafalme 6:15–17. Mwalike mmojawapo wa watoto ajifanye kuwa mtumishi wa Elisha wakati watoto wengine wanauliza maswali kuhusu uzoefu wake, kama vile jinsi alivyohisi wakati jeshi la Shamu lilipozingira mji au ilikuwa vipi kuona jeshi la Mungu. Zungumza na watoto kuhusu nyakati walizohisi kuwa peke yao katika kujaribu kuishi injili. Ni kwa jinsi gani Bwana anatusaidia kujua kwamba hatuko peke yetu?

  • Imbeni wimbo kuhusu kumtegemea Bwana, kama vile “When Faith Endures“ (Nyimbo za Kanisa, na. 128). Ni nini wimbo huu unatufundisha kuhusu kumwamini Bwana?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto washiriki uzoefu pamoja na familia zao wakati walipotambua mkono wa Mungu katika maisha yao. Watie moyo wawaombe wanafamilia wao kushiriki uzoefu sawa na huo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watoto hujifunza kwa njia nyingi. “Juhudi zako katika kuwafundisha watoto zitakuwa za ufanisi zaidi unapotumia mbinu mbali mbali za kufundishia,” ikijumuisha hadithi, picha, na muziki (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25).

Chapisha