Agano la Kale 2022
Julai 18–24. Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–6; 8: “Ninafanya Kazi Kuu”


“Julai 18–24. Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–6; 8: ‘Ninafanya Kazi Kuu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Julai 18–24. Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–6; 8,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
hekalu la Zerubabeli

Mchoro wa hekalu la Zerubabeli, na Sam Lawlor

Julai 18–24

Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–68

“Ninafanya Kazi Kuu”

Unapojifunza, fikiria ni ujumbe gani katika jumbe za Ezra na Nehemia ambazo zinahitajika sana na watoto unaowafundisha. Tengeneza mpango wa kufundisha ambao unajumuisha misukumo unayopokea kutoka kwa Roho Mtakatifu.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Andika ubaoni Zerubabeli, Ezra na Nehemia. Chora au onyesha baadhi ya picha ambazo zinahusika na watu hawa, kama vile hekalu, maandiko, na kuta za Yerusalemu. Wasaidie watoto kuoanisha picha na majina, na waache washiriki kile wanachojua kuhusu kile watu hawa walifanya.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Ezra 3:8–13

Hekalu linaweza kuniletea furaha.

Simulizi ya Zerubabeli na Wayahudi wakijenga hekalu inaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kufurahia baraka ambazo huja kwa sababu ya nyumba ya Bwana.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wazungumze kuhusu kile kinachowapa furaha. Onyesha picha ya mtu akitabasamu mbele ya hekalu (kama vile picha katika muhtasari huu), na uwaulize watoto kwa nini mtu huyu anaonekana kuwa na furaha sana. Shuhudia kwamba hekalu ni nyumba ya Bwana, na waambie kuhusu wakati wewe ulihisi furaha kwa sababu ya hekalu.

  • Wasomee watoto sehemu ya mwisho ya Ezra 3:12, ukielezea kwamba wakati Wayahudi walipoweka msingi wa hekalu, “wengi walipiga kelele za furaha.” Waalike watoto wapige kelele za furaha. Wasaidie kufikiria sababu zinazoweza kutufanya tuwe na furaha kuhusu hekalu. Kwa mfano, katika hekalu tunafanya ahadi na Mungu ambazo zinaruhusu familia zetu kuwa pamoja milele.

  • Imba pamoja na watoto wimbo kuhusu hekalu, kama vile “I Love to See the Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,95). Baada ya kila mstari, simama na umuombe mtoto ashiriki kitu fulani anachokipenda kuhusu hekalu.

    Picha
    familia ikitembea katika eneo la hekalu

    Hekalu linaweza kuwa chanzo cha furaha katika maisha yetu.

Nehemia 2:17–20; 6:1–9

Bwana atanisaidia kufanya kazi Yake.

Wakati Nehemia alipokuwa anakarabati kuta zilizozunguka Yerusalemu, maadui zake walijaribu kumfanya asitishe, lakini yeye alibakia mwaminifu kwenye kazi yake. Ni nini baadhi ya vitu muhimu Bwana anataka watoto wafanye, na ni kwa jinsi gani unaweza kuwatia moyo kuwa waaminifu kwa kazi hiyo?

Shughuli Yamkini

  • Shiriki na watoto hadithi ya Nehemia (ona Nehemia 2:17–20; 6:1–9; Dieter F. Uchtdorf, “We Are Doing a Great Work and Cannot Come Down,” Liahona, Mei 2009, 59–62). Waambie watoto kile Nehemia alisema wakati watu walimkejeli kwa kutaka kutengeneza kuta za Yerusalemu: “Mungu wa mbinguni, yeye atatufanikisha; kwa hiyo sisi, watumishi wake, tutainuka na kujenga” (Nehemia 2:20). Waalike watoto wasimame na kujifanya wanasaidia kutengeneza kuta za Yerusalemu.

  • Lete matofali kadhaa darasani, na waache watoto wayatumie kukusaidia kujenga ukuta (au chora ukuta ubaoni). Wasaidie watoto wafikirie baadhi ya vitu muhimu ambavyo Baba wa Mbinguni anaweza kuwaomba wafanye, kama kujifunza jinsi ya kusoma maandiko. Kwa kila wazo wanaloshiriki, waombe waongeze tofali kwenye ukuta. Elezea kwamba wakati Nehemia alikuwa anafanya kazi yake muhimu ya kutengeneza kuta za Yerusalemu, watu walijaribu kumzuia. Soma Nehemia 6:9, na waalike watoto kuinua mikono yao unaposoma “imarisha mikono yangu.” Waambie watoto kuhusu wakati ambapo ulihisi Mungu akiimarisha mikono yako kufanya kazi Yake.

Nehemia 8:1–12

Maandiko ni baraka.

Unaweza kutumia hadithi ya Ezra akisoma sheria kuwasaidia watoto kufikiria kuhusu jinsi tulivyobarikiwa kwa kuwa na maandiko.

Shughuli Yamkini

  • Waambie watoto kwamba Ezra aliwasomea watu maandiko. Soma kwa sauti vifungu vya maneno kutoka Nehemia 8:2–3, 5–6, 8–9, 12 ambavyo vinaeleza kile watu walichofanya waliposikia maandiko, na uwaalike watoto waigize vifungu hivi vya maneno. Kwa nini tuna shukurani kwa kuwa maandiko?

  • Waalike watoto kupaka rangi ukurasa wa shughuli ya wiki hii. Wakati wakifanya hilo, shiriki na watoto jinsi kusoma maandiko kulivyokuleta karibu kwa Mwokozi.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Ezra 3:8–13; 6:16–22

Hekalu hunipa sababu ya kufurahi.

Unaporejelea pamoja na watoto simulizi ya Zerubabeli na Wayahudi wakifanya ukarabati wa hekalu, tafuta njia za kushuhudia juu ya furaha ambayo huja kwetu kwa sababu tuna mahekalu leo.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wafanye kazi pamoja kutafuta vifungu vya maneno katika Ezra 3:10–13 ambavyo vinaonyesha jinsi Wayahudi walivyohisi wakati hekalu katika Yerusalemu lilikuwa linafanyiwa ukarabati. Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kuonyesha furaha yetu kwa kuwa na mahekalu hapa duniani leo? Wasaidie watoto kufikiria njia wanazoweza kujiandaa kwenda hekaluni.

  • Shiriki na watoto hisia zako kuhusu hekalu. Je, hekalu limekusaidia vipi kuhisi kuwa karibu na Baba wa Mbinguni na Mwokozi? Kwa nini tunasherehekea wakati hekalu linapowekwa wakfu? Wape watoto muda wa kuandika jinsi wanavyohisi kuhusu hekalu, na uwatie moyo kushiriki kile walichoandika na familia zao.

Nehemia 2; 46

Bwana ataniimarisha kufanya “kazi kuu.”

Bwana ana kazi muhimu kwa ajili ya watoto unaowafundisha. Wanaweza kujifunza nini kutoka kwa Nehemia kuhusu kustahimili katika kazi hiyo hata wakati wanapokabiliana na upinzani?

Shughuli Yamkini

  • Pitia tena pamoja na watoto hadithi kuhusu Nehemia akikarabati kuta zinazozingira Yerusalemu, ikijumuisha upinzani uliomkabili. Someni pamoja Nehemia 2:19, na waombe watoto washiriki hali ambazo mtu angeweza kutucheka kwa kufanya kitu sahihi. Kulingana na Nehemia 2:20, je, Nehemia alijibu vipi? Tunaweza kujibu vipi wakati watu wanatukejeli au kutukosoa kwa kufanya kitu sahihi?

  • Someni pamoja Nehemia 6:1–9. Ni kwa jinsi gani maadui wa Nehemia walijaribu mara kwa mara kumfanya aachane na kazi ya ukuta, na yeye alijibu vipi? Ni kazi gani Mungu anataka sisi tufanye? (ona kwa mfano, Mosia 18:8–10). Tunawezaje kuufuata mfano wa Nehemia katika mstari wa 9 wakati ni vigumu kufanya kile Mungu ametutaka tufanye?

Nehemia 8:1–12

Ninabarikiwa wakati ninapojifunza maandiko.

Watu wa Yerusalemu hawakuwa wamesikia maneno ya Mungu kwa muda mrefu kabla ya Ezra kuwasomea watu. Hadithi ya Ezra inatukumbusha jinsi maandiko yanavyopaswa kuwa muhimu kwetu.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wapekue Nehemia 8:1–12 na watafute maneno na vifungu vya maneno ambavyo vinaonyesha jinsi watu walivyohisi kuhusu kusikia neno la Mungu. Waombe watoto washiriki jinsi wanavyohisi wanapokuwa wakisoma maandiko, na kushiriki hisia zako pia.

  • Mwalike mtoto asome Nehemia 8:8, na waulize watoto kile kinachowasaida kuelewa maandiko. Waonyeshe jinsi ya kutumia visaidizi vya kujifunza maandiko kama vile Mwongozo wa Maandiko na Mada za Injili (ChurchofJesusChrist.org). Waalike watoto washiriki kitu walichojifunza kuhusu Mwokozi kutoka kwenye maandiko.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto wachague kitu walichojifunza leo ambacho wangependa kushiriki pamoja na familia zao.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Jiandae kiroho. “Ufundishaji injili wenye nguvu haumaanishi tu kuandaa somo bali pia kujiandaa sisi wenyewe. … Walimu wa injili wenye tija—kabla hawajafikiria kuhusu kujaza muda wa darasani—hufokasi kwenye kujaza mioyo yao na Roho Mtakatifu” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 12).

Chapisha